
Anwani za makazi zaboresha usafirishaji wa dawa na vifaa vya shule nchini
Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe. Dkt. Festo Dugange, amesema kuwa mfumo wa anwani za makazi umeleta mapinduzi makubwa katika usambazaji wa dawa kwenye vituo vya kutolea huduma za afya ya msingi nchini, kwani hakuna tena changamoto ya kutafuta au kuuliza eneo la zahanati au kituo cha afya kilipo.
Akizungumza leo Februari 8, 2025 kwenye kilele cha maadhimisho ya Wiki ya Anwani za Makazi jijini Dodoma, Dkt. Dugange ameeleza kuwa pamoja na dawa, mfumo huu pia umewezesha vifaa na mahitaji muhimu ya shule kufikishwa katika maeneo husika kwa ufanisi mkubwa zaidi kuliko ilivyokuwa kabla ya utekelezaji wa mfumo huo.
Aidha, amebainisha kuwa Bohari ya Dawa ya Taifa (MSD) sasa inasambaza dawa moja kwa moja hadi kwenye zahanati katika maeneo yote ya Tanzania kwa kutumia anwani za makazi, jambo ambalo limeimarisha usambazaji wa dawa na huduma za afya kwa wananchi wa mijini na vijijini kwa kiwango kikubwa.
Dkt. Dugange amesisitiza kuwa mfumo wa anwani za makazi umewezesha maeneo yote nchini kufikika kwa urahisi zaidi, na Ofisi ya Rais - TAMISEMI itaendelea kusimamia na kuhakikisha utekelezaji wake unazidi kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi.
Comments
Please sign in to leave a comment.
Tangazo la kuitwa kazini ajira za TMCHIP 2025
Mpango Mkakati wa Usimamizi wa Takwimu wa Ofisi ya Rais TAMISEMI - 2024/25 -2028/29
Kanuni za Uchaguzi wa Mwenyekiti wa Kitongoji 2024
Kanuni za Uchaguzi wa mwaka 2024
Tangazo la Uchaguzi




