Recent Updates

Mchengerwa: tuulinde muungano kwa vizazi vyetu
OR-TAMISEMI
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa ametoa wito kwa Watanzania kuuenzi Muungano kwa ajili ya kudumisha amani, umoja na udugu huku akipendekeza kuanzishwa kwa wiki maalum ya Muungano kwa shule zote nchini ili kukuza uelewa wa wanafunzi kuhusu historia ya Muungano.
Mhe.Mchengerwa ameyasema hayo katika kijiji cha Sangambi mkoani Mbeya baada ya kukagua na kuweka mawe ya msingi kwenye miradi ya maendeleo yenye thamani ya Sh.bilioni 40 huku wananchi wakimpongeza Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan kwa uwekezaji mkubwa.
Amehamasisha wasanii na waandishi kuendeleza simulizi za mshikamano wa kitaifa ili kudumisha Muungano huku akiwaasa wazazi kuwaelimisha vijana juu ya thamani ya Muungano.
Amesisitiza kuwa Tanzania ni mfano wa amani barani Afrika, tofauti na mataifa mengine yaliyogubikwa na migogoro na kwamba Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ulikuwa wa kweli, wa kiitikadi na kimaadili, na umeleta mafanikio makubwa kwa taifa.
Waziri Mchengerwa ampongeza Rais Samia kama alama ya mafanikio ya Muungano, akisema kuwa Tanzania imekuwa ya kwanza Afrika Mashariki kumpa mwanamke nafasi ya urais, jambo ambalo hata mataifa makubwa hayajafanikisha.

Kemikali za maabara kwenye shule za sekondari kuwa za uhakika.
OR-TAMISEMI
Serikali itaendelea kuimarisha Mipango na Bajeti kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya maabara na kemikali za maabara ili kuhakikisha vinapatikana kwa uhakika na wakati kwa ajili ya ujifunzaji na kufundishia.
Haya yamebainishwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mhe Mohamed Mchengerwa wakati wa kujibu hoja za wabunge kuhusu mpango wa Serikali wa kupeleka vifaa vya maabara kwenye shule 26 za sayansi za wasichana za mikoa, bila kuathiri mipango iliypowekwa ya upelekaji wa vifaa vya maabara katika shule nyingine za sekondari nchini.
Amesema vifaa vya maabara kwa shule 486 vimenunuliwa katika awamu mbili (2) na usambazaji wa awamu ya kwanza unahusisha shule 231, zikiwemo shule 26 za sayansi za wasichana na hadi sasa shule 8 kati 26 za wasichana zimepokea vifaa hivyo na usambazaji katika shule 18 zilizobakia unaendelea.
Amesema vifaa vya maabara na kemikali kwa awamu ya pili kwa ajili ya shule 255 zilizobaki vinaendelea kupokelewa na kusambazwa na pia Serikali imenunua na kusambaza kemikali za maabara katika shule za sekondari 231 ngazi ya kata.
Kuhusu kubuni chanzo cha kudumu cha fedha kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya maabara kwa shule za sekondari nchini, Mchengerwa amesema Serikali imekuwa ikitoa fedha za ununuzi wa vifaa vya maabara kwa shule za sekondari nchini kupitia Ruzuku ya Uendeshaji wa Shule.
Pia ununuzi wa vifaa vya maabara hufanyika kupitia utekelezaji wa miradi mbalimbali ikiwemo Mradi wa Kuimarisha Elimu ya Sekondari (SEQUIP), Mpango wa Lipa kulingana na Matokeo (EP4R) na michango ya wadau.
Hivyo, Mchengerwa amesema Serikali itaendelea kuimarisha Mipango na Bajeti kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya maabara na kemikali za maabara ili kuhakikisha vinapatikana kwa uhakika na wakati kwa ajili ya ujifunzaji na kufundishia.
Kuhusu hoja ya usimamizi na uendeshaji wa shule za mchepuo wa kiingereza katika halmashauri, Mchengerwa amesema Ofisi ya Rais - TAMISEMI imeipokea hoja hii na itafanya uchambuzi kwa kushirikiana na Wizara inayosimamia Sera ya Elimu ili kupata utekelezaji mzuri wahojahusika.

Wakurugenzi wa halmashauri waelekezwa kuwasilisha majina ya watumishi wanaodai malimbikizo
OR-TAMISEMI
Naibu Waziri Ofisi ya Rais – TAMISEMI Mhe. Zainab Katimba amewaelekeza wakurugenzi wa Mamlaka za serikali za mitaa kutengeneza mchanganuo na kubaini watumishi wangapi wanadai malimbikizo ya mishahara na yasiyo yamishahara na kuyawasilisha Utumishi kuhakikiwa na kupekwa hazina kwaajili ya malipo.
Ameyatoa maelekezo hayo bungeni Dodoma wakati akijibu swali la Mhe. Bonnah Kamoli mbunge wa Segerea kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais – TAMISEMI Mhe. Mohamed Mchengerwa, aliyetaka kujua serikali inampango gani wa kulipa malimbikizo ya mishahara na marupurupu ya walimu.
Akijibu hilo Mhe. Katimba amesema “Naomba nitoe msisitizo huo na jana kwenye bajeti ya wizara ya utumishi maelekezo hayo yalitolewa na wizara hiyo na mpaka itakapo fika tarehe 31 Mei wakurugenzi wote wawe wamewasilisha majina hayo ya watumishi hao ambao wanadai malipo yao” Amesema
Aidha, akijibu kuhusu mazingira bora ya walimu Mhe. Katimba amesema serikali inaendelea kujenga nyumba za walimu ili walimu wapate mazingira mazuri ya kuishi na kufanyakazi kwa ufanisi.

Serikali kudhibiti madeni mapya ya watumishi
OR-TAMISEMI
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mhe Mohamed Mchengerwa amesema Serikali imeendelea kudhibiti uzalishaji wa madeni mapya ya kimshahara na yasiyo ya kimshahara.
Mchengewa ameyasema hayo wakati wa kujibu hoja kuhusu Serikali kulipa kwa wakati madeni mbalimbali ya watumishi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa nchini ili kuondoa malimbikizo ya madeni.
Amesema Serikali imeendelea kulipa madeni ya watumishi wa mamlaka za serikali za mitaa na katika mwaka 2023/24 Shilingi bilioni 116.08 zimetolewa kwa ajili ya kulipa madeni ya watumishi ambapo, mishahara ni Shilingi bilioni 32.22 na madeni yasiyo ya mishahara ni shilingi bilioni 83.85.
Amefafanua kuwa katika mwaka 2024/25 hadi machi, 2025 madeni yenye thamani ya Shilingi bilioni 78.75 yamelipwa, kati yake Sh bilioni 16.32 ni madeni ya mshahara na shilingi bilioni 62.43 ni madeni yasiyo ya mshahara yanayojumuisha fedha za uhamisho, likizo na stahiki za watumishi.
Mchengerwa amesema katika kuendelea kuhakikisha madeni yanaendelea kulipwa, Ofisi ya Rais-TAMISEMI kupitia Ofisi za Wakuu wa Mikoa imekamilisha zoezi la uhakiki wa madeni ya watumishi yasiyo ya mishahara kufikia juni 2024 ambapo Halmashauri 36 zimeonekana zinaweza kulipa zenyewe kutokana na mapato yao ya ndani na 145 hazina uwezo.
“Taarifa ya uhakiki imewasilishwa Wizara ya Fedha kwa ajili ya kuendelea na hatua zinazofuata.”amesema Mchengerwa
Aidha, Mchengerwa amesema Serikali imedhibiti uzalishaji wa madeni mapya ya kimshahara kwa kuingiza kwa wakati watumishi wote wanaoajiriwa kwa mara ya kwanza katika payroll ya Serikali, kuhakikisha marekebisho ya mishahara yanafanyika kabla ya mtumishi kupata barua ya kupanda daraja na kuingizwa kwenye payroll ya Serikali posho za watumishi wanaokaimu madaraka.
Pia katika kudhibiti uzalishaji wa madeni yasiyo ya kimshahara Serikali imeyadhibitiwa kwa kutoa ruzuku kwa ajili ya gharama za likizo, uhamisho na stahiki za viongozi.

Bunge lapitisha kwa kishindo bajeti ya tamisemi trilioni 11.78 kwa mwaka 2025/2026
Na Mwandishi Wetu, bungeni Dodoma
Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wamepitisha kwa kauli moja bajeti ya Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kwa mwaka wa fedha 2025/26 yenye takribani Shilingi trilioni 11. 783 kwa ajili ya wizara na taasisi zilizo chini yake.
Kwa mujibu wa Waziri Mchengerwa Bajeti hiyo imeongezeka kutoka Shilingi trilioni 10.125 zilizotengwa mwaka 2024/25 hadi kufikia Shilingi trilioni 11.783 na kuwa na ongezeko la zaidi ya Sh trilioni 1.66.
Shilingi trilioni 3.95 zimepitishwa kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo ambapo kati ya fedha hizo Shilingi trilioni 2.5 ni fedha za ndani, ikijumuisha Shilingi bilioni 613.44 za mapato ya ndani ya halmashauri na Shilingi trilioni 1.45 ni fedha za nje.
Pia Shilingi trilioni 7.84 ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida yanayojumuisha mishahara Shilingi trilioni 6.3 na matumizi mengineyo Shilingi trilioni 1.53 ikijumuisha Shilingi trilioni 1. 067 za mapato ya ndani ya halmashauri.
Akijibu hoja za wabunge Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe Mohamed Mchengerwa amesema kuwa anatambua uwepo wa changamoto za ujenzi, ukarabati na matengenezo ya barabara katika maeneo mbalimbali nchini. Katika kushughulikia changamoto hiyo serikali imeendelea kutenga fedha kupitia TARURA kwa ajili ya ujenzi, matengenezo na ukarabati wa Barabara ambapo bajeti imeongezeka kutoka shilingi bilioni 275.00 mwaka 2020/21 hadi shilingi bilioni 772.19 mwaka 2024/25 sawa na ongezeko la asilimia 180.8 ya fedha za ndani.
Pia Waziri Mchengerwa amesema kuwa Ofisi ya Rais - TAMISEMI inatambua umuhimu wa kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia ambapo imeendelea kujenga na kukarabati miundombinu ya elimu pamoja na kuendeleza mazingira ya maeneo hayo.
Serikali imeendelea kuwekeza katika utoaji wa Elimumsingi na Sekondari ambapo Mpango wa Elimumsingi bila Ada umeongezewa bajeti yake kutoka shilingi bilioni 249.66 mwaka 2020/21 hadi shilingi bilioni 510.96 mwaka 2025/26 kwa mwaka sawa na ongezeko la shilingi bilioni 261.30 sawa na asilimia 104.66.
Waziri Mchengerwa ametoa maelekezo kwa wakuu wa mikoa na Wilaya: kujikita kikamilifu katika kulinda amani, mshikamano wa kitaifa na ufanisi wa utendaji wa serikali katika maeneo yao.
”Hamtakiwi kuwa watazamaji wa migogoro—bali wazima moto wa chokochoko, na walinzi wa misingi ya haki, maendeleo na umoja wa kitaifa” Amesisitiza Waziri Mchengerwa
Na kuongeza kuwa Utulivu wa nchi unaanza pale ambapo viongozi wa chini wanatimiza wajibu wao bila kusubiri maagizo kutoka juu.
News Archive

Mchengerwa: tuulinde muungano kwa vizazi vyetu
OR-TAMISEMI
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa ametoa wito kwa Watanzania kuuenzi Muungano kwa ajili ya kudumisha amani, umoja na udugu huku akipendekeza kuanzishwa kwa wiki maalum ya Muungano kwa shule zote nchini ili kukuza uelewa wa wanafunzi kuhusu historia ya Muungano.
Mhe.Mchengerwa ameyasema hayo katika kijiji cha Sangambi mkoani Mbeya baada ya kukagua na kuweka mawe ya msingi kwenye miradi ya maendeleo yenye thamani ya Sh.bilioni 40 huku wananchi wakimpongeza Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan kwa uwekezaji mkubwa.
Amehamasisha wasanii na waandishi kuendeleza simulizi za mshikamano wa kitaifa ili kudumisha Muungano huku akiwaasa wazazi kuwaelimisha vijana juu ya thamani ya Muungano.
Amesisitiza kuwa Tanzania ni mfano wa amani barani Afrika, tofauti na mataifa mengine yaliyogubikwa na migogoro na kwamba Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ulikuwa wa kweli, wa kiitikadi na kimaadili, na umeleta mafanikio makubwa kwa taifa.
Waziri Mchengerwa ampongeza Rais Samia kama alama ya mafanikio ya Muungano, akisema kuwa Tanzania imekuwa ya kwanza Afrika Mashariki kumpa mwanamke nafasi ya urais, jambo ambalo hata mataifa makubwa hayajafanikisha.

Kemikali za maabara kwenye shule za sekondari kuwa za uhakika.
OR-TAMISEMI
Serikali itaendelea kuimarisha Mipango na Bajeti kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya maabara na kemikali za maabara ili kuhakikisha vinapatikana kwa uhakika na wakati kwa ajili ya ujifunzaji na kufundishia.
Haya yamebainishwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mhe Mohamed Mchengerwa wakati wa kujibu hoja za wabunge kuhusu mpango wa Serikali wa kupeleka vifaa vya maabara kwenye shule 26 za sayansi za wasichana za mikoa, bila kuathiri mipango iliypowekwa ya upelekaji wa vifaa vya maabara katika shule nyingine za sekondari nchini.
Amesema vifaa vya maabara kwa shule 486 vimenunuliwa katika awamu mbili (2) na usambazaji wa awamu ya kwanza unahusisha shule 231, zikiwemo shule 26 za sayansi za wasichana na hadi sasa shule 8 kati 26 za wasichana zimepokea vifaa hivyo na usambazaji katika shule 18 zilizobakia unaendelea.
Amesema vifaa vya maabara na kemikali kwa awamu ya pili kwa ajili ya shule 255 zilizobaki vinaendelea kupokelewa na kusambazwa na pia Serikali imenunua na kusambaza kemikali za maabara katika shule za sekondari 231 ngazi ya kata.
Kuhusu kubuni chanzo cha kudumu cha fedha kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya maabara kwa shule za sekondari nchini, Mchengerwa amesema Serikali imekuwa ikitoa fedha za ununuzi wa vifaa vya maabara kwa shule za sekondari nchini kupitia Ruzuku ya Uendeshaji wa Shule.
Pia ununuzi wa vifaa vya maabara hufanyika kupitia utekelezaji wa miradi mbalimbali ikiwemo Mradi wa Kuimarisha Elimu ya Sekondari (SEQUIP), Mpango wa Lipa kulingana na Matokeo (EP4R) na michango ya wadau.
Hivyo, Mchengerwa amesema Serikali itaendelea kuimarisha Mipango na Bajeti kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya maabara na kemikali za maabara ili kuhakikisha vinapatikana kwa uhakika na wakati kwa ajili ya ujifunzaji na kufundishia.
Kuhusu hoja ya usimamizi na uendeshaji wa shule za mchepuo wa kiingereza katika halmashauri, Mchengerwa amesema Ofisi ya Rais - TAMISEMI imeipokea hoja hii na itafanya uchambuzi kwa kushirikiana na Wizara inayosimamia Sera ya Elimu ili kupata utekelezaji mzuri wahojahusika.

Wakurugenzi wa halmashauri waelekezwa kuwasilisha majina ya watumishi wanaodai malimbikizo
OR-TAMISEMI
Naibu Waziri Ofisi ya Rais – TAMISEMI Mhe. Zainab Katimba amewaelekeza wakurugenzi wa Mamlaka za serikali za mitaa kutengeneza mchanganuo na kubaini watumishi wangapi wanadai malimbikizo ya mishahara na yasiyo yamishahara na kuyawasilisha Utumishi kuhakikiwa na kupekwa hazina kwaajili ya malipo.
Ameyatoa maelekezo hayo bungeni Dodoma wakati akijibu swali la Mhe. Bonnah Kamoli mbunge wa Segerea kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais – TAMISEMI Mhe. Mohamed Mchengerwa, aliyetaka kujua serikali inampango gani wa kulipa malimbikizo ya mishahara na marupurupu ya walimu.
Akijibu hilo Mhe. Katimba amesema “Naomba nitoe msisitizo huo na jana kwenye bajeti ya wizara ya utumishi maelekezo hayo yalitolewa na wizara hiyo na mpaka itakapo fika tarehe 31 Mei wakurugenzi wote wawe wamewasilisha majina hayo ya watumishi hao ambao wanadai malipo yao” Amesema
Aidha, akijibu kuhusu mazingira bora ya walimu Mhe. Katimba amesema serikali inaendelea kujenga nyumba za walimu ili walimu wapate mazingira mazuri ya kuishi na kufanyakazi kwa ufanisi.

Serikali kudhibiti madeni mapya ya watumishi
OR-TAMISEMI
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mhe Mohamed Mchengerwa amesema Serikali imeendelea kudhibiti uzalishaji wa madeni mapya ya kimshahara na yasiyo ya kimshahara.
Mchengewa ameyasema hayo wakati wa kujibu hoja kuhusu Serikali kulipa kwa wakati madeni mbalimbali ya watumishi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa nchini ili kuondoa malimbikizo ya madeni.
Amesema Serikali imeendelea kulipa madeni ya watumishi wa mamlaka za serikali za mitaa na katika mwaka 2023/24 Shilingi bilioni 116.08 zimetolewa kwa ajili ya kulipa madeni ya watumishi ambapo, mishahara ni Shilingi bilioni 32.22 na madeni yasiyo ya mishahara ni shilingi bilioni 83.85.
Amefafanua kuwa katika mwaka 2024/25 hadi machi, 2025 madeni yenye thamani ya Shilingi bilioni 78.75 yamelipwa, kati yake Sh bilioni 16.32 ni madeni ya mshahara na shilingi bilioni 62.43 ni madeni yasiyo ya mshahara yanayojumuisha fedha za uhamisho, likizo na stahiki za watumishi.
Mchengerwa amesema katika kuendelea kuhakikisha madeni yanaendelea kulipwa, Ofisi ya Rais-TAMISEMI kupitia Ofisi za Wakuu wa Mikoa imekamilisha zoezi la uhakiki wa madeni ya watumishi yasiyo ya mishahara kufikia juni 2024 ambapo Halmashauri 36 zimeonekana zinaweza kulipa zenyewe kutokana na mapato yao ya ndani na 145 hazina uwezo.
“Taarifa ya uhakiki imewasilishwa Wizara ya Fedha kwa ajili ya kuendelea na hatua zinazofuata.”amesema Mchengerwa
Aidha, Mchengerwa amesema Serikali imedhibiti uzalishaji wa madeni mapya ya kimshahara kwa kuingiza kwa wakati watumishi wote wanaoajiriwa kwa mara ya kwanza katika payroll ya Serikali, kuhakikisha marekebisho ya mishahara yanafanyika kabla ya mtumishi kupata barua ya kupanda daraja na kuingizwa kwenye payroll ya Serikali posho za watumishi wanaokaimu madaraka.
Pia katika kudhibiti uzalishaji wa madeni yasiyo ya kimshahara Serikali imeyadhibitiwa kwa kutoa ruzuku kwa ajili ya gharama za likizo, uhamisho na stahiki za viongozi.

Bunge lapitisha kwa kishindo bajeti ya tamisemi trilioni 11.78 kwa mwaka 2025/2026
Na Mwandishi Wetu, bungeni Dodoma
Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wamepitisha kwa kauli moja bajeti ya Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kwa mwaka wa fedha 2025/26 yenye takribani Shilingi trilioni 11. 783 kwa ajili ya wizara na taasisi zilizo chini yake.
Kwa mujibu wa Waziri Mchengerwa Bajeti hiyo imeongezeka kutoka Shilingi trilioni 10.125 zilizotengwa mwaka 2024/25 hadi kufikia Shilingi trilioni 11.783 na kuwa na ongezeko la zaidi ya Sh trilioni 1.66.
Shilingi trilioni 3.95 zimepitishwa kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo ambapo kati ya fedha hizo Shilingi trilioni 2.5 ni fedha za ndani, ikijumuisha Shilingi bilioni 613.44 za mapato ya ndani ya halmashauri na Shilingi trilioni 1.45 ni fedha za nje.
Pia Shilingi trilioni 7.84 ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida yanayojumuisha mishahara Shilingi trilioni 6.3 na matumizi mengineyo Shilingi trilioni 1.53 ikijumuisha Shilingi trilioni 1. 067 za mapato ya ndani ya halmashauri.
Akijibu hoja za wabunge Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe Mohamed Mchengerwa amesema kuwa anatambua uwepo wa changamoto za ujenzi, ukarabati na matengenezo ya barabara katika maeneo mbalimbali nchini. Katika kushughulikia changamoto hiyo serikali imeendelea kutenga fedha kupitia TARURA kwa ajili ya ujenzi, matengenezo na ukarabati wa Barabara ambapo bajeti imeongezeka kutoka shilingi bilioni 275.00 mwaka 2020/21 hadi shilingi bilioni 772.19 mwaka 2024/25 sawa na ongezeko la asilimia 180.8 ya fedha za ndani.
Pia Waziri Mchengerwa amesema kuwa Ofisi ya Rais - TAMISEMI inatambua umuhimu wa kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia ambapo imeendelea kujenga na kukarabati miundombinu ya elimu pamoja na kuendeleza mazingira ya maeneo hayo.
Serikali imeendelea kuwekeza katika utoaji wa Elimumsingi na Sekondari ambapo Mpango wa Elimumsingi bila Ada umeongezewa bajeti yake kutoka shilingi bilioni 249.66 mwaka 2020/21 hadi shilingi bilioni 510.96 mwaka 2025/26 kwa mwaka sawa na ongezeko la shilingi bilioni 261.30 sawa na asilimia 104.66.
Waziri Mchengerwa ametoa maelekezo kwa wakuu wa mikoa na Wilaya: kujikita kikamilifu katika kulinda amani, mshikamano wa kitaifa na ufanisi wa utendaji wa serikali katika maeneo yao.
”Hamtakiwi kuwa watazamaji wa migogoro—bali wazima moto wa chokochoko, na walinzi wa misingi ya haki, maendeleo na umoja wa kitaifa” Amesisitiza Waziri Mchengerwa
Na kuongeza kuwa Utulivu wa nchi unaanza pale ambapo viongozi wa chini wanatimiza wajibu wao bila kusubiri maagizo kutoka juu.

Wabunge waitaka wizara ya fedha iipe fedha wizara ya tamisemi itekeleze majukumu yake
Na Mwandishi wetu, Dodoma
WABUNGE mbalimbali wameipongeza Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kwa ufanisi wao ambao wamekuwa wakiufanya katika kuhakikisha miundombinu, elimu, afya na mambo mengine yanafanyika kwa ustadi mkubwa.
Akichangia bungeni bajeti ya TAMISEMI kwa mwaka wa fedha 2025/2026 Mbunge wa jimbo la Korogwe Vijijini Mhe Timotheo Mnzava amesema kuwa anakubaliana na kazi kubwa ambayo imekuwa ikifanywa na TARURA huku akisema kuwa wanmaiomba wizara ya fedha iwapelekee TAMISEMI, Tarura fedha ili waweze kutatua changamoto zilizopo.
“Tunaipongeza serikali kwa kipindi cha miaka minne mitano tumefanya kazi kubwa sana na serikali imeleta fedha nyingi sana kuunga mkono ujengaji wa maboma ya madarasa na zahanati” Amekaririwa Mnzava
Naye Mbunge wa Jimbo la Sengerema Mhe Hamis Tabasam amesema kuwa serikali za mitaa imebeba maslahi makubwa ya wananchi na kusema kuwa sengerema walikuwa wana matatizo ya shule za sekondari, shule za msingi Barabara na hata huduma za afya.
“Lakini katika kipindi hiki cha miaka minne Rais Dk. Samia Suluhu Hassan amefanya kazi kubwa kuhakikisha huduma za kijamii katika nchi hii zinaboreshwa kwa kiwango kikubwa”amesema.
Jambo hili linatutolea hofu kwa sisi wabunge hakuna mbunge ambaye atakuwa na mashaka yakutokuchaguliwa jimboni kwake labda kama anahali mbaya damu zimechafuka tu maana kila kitu kipo vizuri kwa sasa.
Hata hivyo naye Mbunge wa jimbo la Nyamagana Mhe Stansilaus Mabula amesema kuwa kumekuwa na utulivu wa kiwango cha hali ya juu wizara ya TAMISEMI tangu alipoteuliwa Waziri Mhe Mohammed Mchengerwa .
Tunaposema hakuna kilichosimama hakika tunamaanisha kwasababu yote yanayojitokeza ni mambo ambayo yamejitokeza kwa muda mfupi na yameleta tija kwa watanzania.
“Tunapozungumzia uboreshaji wa sekta ya elimu msingi na sekondari namna ambavyo shule za msingi na sekondari zimeboreka.
Leo tunapozungumza kwenye uboreshaji wa shule za msingi zinazozingatia takwa maalum la Watoto wadogo (kindergarten) kupata eneo la kujifunzia hili nijambo kubwa sana na lenye tija katika nchi yetu.

Mchengerwa- marc, madc imsiwe watazamaji wa migogoro
OR-TAMISEMI
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa ametoa maelekezo mahususi kwa wakuu wa mikoa na wa wilaya akiwataka kutokuwa watazamaji wa migogoro na walinzi wa misingi ya haki na amani.
Mchengerwa ameyasema hayo wakati akihitimisha hoja ya mapato na matumizi ya Ofisi ya Rais-TAMISEMI na taasisi zake, Tume ya Utumishi wa Walimu, Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa mwaka 2024/25.
“Ninapenda pia kutumia nafasi hii kutoa maelekezo mahsusi kwa Wakuu wa Mikoa na Wilaya, wajikite kikamilifu katika kulinda amani, mshikamano wa kitaifa na ufanisi wa utendaji wa serikali katika maeneo yao.”
“Hamtakiwi kuwa watazamaji wa migogoro bali wazima moto wa chokochoko, na walinzi wa misingi ya haki, maendeleo na umoja wa kitaifa. Utulivu wa nchi unaanza pale ambapo viongozi wa chini wanatimiza wajibu wao bila kusubiri maagizo kutoka juu.” amesema Mchengerwa
Amewataka kuwasha mwenge wa ulinzi wa jamii na kuzima cheche za migogoro midogo inayoweza kuwa moto mkubwa wa Taifa.

Bil. 66.57/- kujenga matundu ya vyoo 28,580
OR-TAMISEMI
KATIKA mwaka 2025/26, Serikali imetenga Sh.Bilioni 66.57 kwa ajili ya kujenga matundu 28,580 ya vyoo katika shule za msingi na sekondari.
Akijibu hoja ya wabunge kuhusu serikali kufanya tathimini ya kubaini ubora na ukubwa wa tatizo la upungufu wa matundu ya vyoo katika shule zote za msingi na sekondari, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mohamed Mchengerwa amesema Serikali inatambua umuhimu wa kulinda afya za walimu na wanafunzi, hivyo itaendelea kukabiliana na changamoto hiyo kwa lengo la kulinda utu na afya za wanafunzi.
Amesema Sensa ya Elimumusingi ya mwaka 2024 inaonesha mahitaji ya matundu ya vyoo katika shule za msingi ni 429,599 wakati yaliyopo ni matundu 240,320, hivyo kuwa na upungufu kuwa ni matundu 189,279, hivyo kufanya wastani wa uwiano kwa wavulana ni 1:47 badala ya 1:25 unaohitajika na kwa wasichana kuwa ni 1:43 badala ya 1:20.
Kwa upande wa sekondari, mahitaji ni matundu 135,870 wakati yaliyopo ni matundu 84,608 na upungufu ni matundu 51,262, hivyo kufanya wastani wa uwiano uliopo kwa wavulana ni 1:36 badala ya 1:25 na wasichana ni 1:35 badala ya 1:20.
Aidha, Mchengerwa amesema mkakati wa Serikali ni kufanya tathmini ya ubora wa ujenzi wa matundu ya vyoo na kuendelea kutenga fedha kila mwaka kwa ajili ya ujenzi wa matundu ya vyoo kwa shule za msingi na sekondari na kuhakikisha kuwa kwa sasa kila darasa linalojengwa kunakuwa na ujenzi wa angalau matundu mawili ya vyoo.
“Katika mwaka 2025/26, Serikali imepanga kujenga matundu 28,580 ya vyoo yatakayogharimu shilingi bilioni 66.57 katika shule za msingi na sekondari.”
Mchengerwa ameongeza kuwa: choo cha staha ni haki ya mwanafunzi; ni chozi lisiloonekana, lakini lenye kuumiza.”
“Tuwashe mwenge wa heshima shuleni-tuzime giza la aibu ya vyoo visivyofaa...Serikali haijalala katika hili, lengo ni kuhakikisha shule zetu zinakuwa mahali salama pa fundishia na kujifunzia," amesema.

Wananchi dodoma waipa heko bajeti ya tamisemi
Na Mwandishi Wetu, Dodoma
Ikiwa leo ni siku ya mwisho ya kujadiliwa kwa bajeti ya Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) wananchi mkoani Dodoma wamejitokeza kutoa maoni yao kuhusu bajeti hiyo kwa mwaka wa fedha 2025/2026 yenye kiasi cha shilingi bilioni 11.7.
Akizunguzmia bajaeti hiyo mkazi wa Dodoma Bi Maria Julias ambaye pia ni fundi cherehani amesema kuwa anatamani bajeti ya TAMISEMI ilenge zaidi kwenye TEHAMA ambapo itawarahisishia wafanyabiashara kwani dunia ipo kiganjani hivyo inawarahisishia wafanyabiashara kujitangaza kupitia mitandao ya kijamii.
“Mfano mimi nikishona nguo zangu huwa naweka kwenye mitandao ya kijamii kwahiyo natumai tamisemi itatusaidia kwa upande huo”amesema Maria
Kwa upande wake Emmanuel Mabalwe amesema kuwa amefuatilia Bunge na kuona bajeti ya Tamisemi kwa mwaka wa fedha 2025/2026 iliyowasilishwa na Waziri wa TAMISEMI Mhe Mohammed Mchengerwa.
Amesema kuwa bajeti ya mwaka huu ya Tamisemi kwa mwaka wa fedha 2025/2026 imekuwa na ongezeko kwa kiasi kikubwa kutoka bajeti ya mwaka jana 2024/2025 ambayo ilikuwa ya tril.10.1 hadi kiasi cha tril 11.7
“Kwahiyo ongezeko ni kubwa ambapo Trilioni 1.66 ndiyo ambayo imeongezeka kwa mwaka huu na hiki ni kiwango kikubwa ambacho kitaenda kuhudumia watanzania” Amesema.
Naye Manoa Samweli amesema bajeti ya TAMISEMI ijikite kwenye masuala ya michezo kwani mpaka sasa michezo imekuwa ajira kwa vijana wengi ambao wana kipaji.
Amesema mchezo wa mpira wa miguu lunazidi kukua hivyo inatakiwa kuwepo na maboresho zaidi hasa kwenye miundombinu ya michezo kama vile viwanja jambo litakalosaidia kuweka ajira na kupata ajira kwa vijana ambao wana vipaji vya mpira.

Wazee rufiji wamuombea dua waziri mchengerwa
OR-TAMISEMI
Wazee Wilayani Rufiji wamefanya Dua ya kumuombea Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Rufiji Mhe. Mohamed Mchengerwa ya kumtakia heri katika utekelezaji wa majukumu yake ya kitaifa pamoja na jukumu la kuijenga Rufiji kupitia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo
Dua hiyo imefanyika katika Msikiti Mkuu wa Jumuiya ya Ikwiriri na Mitaa mbalimbali ya Ikwiriri, ambapo wananchi wa Rufiji wamepata fursa ya kuwaombea waliotangulia mbele za haki, kuliombea Taifa liendelee kuwa na amani na utulivu, pamoja na kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan na viongozi aliwateua ili waendelee kulitumia taifa kwa uzalendo.
Wakizungumza katika Mahojiano Maalumu Wazee hao, akiwemo Daruesh Rwanda Mkazi wa Ikwiriri amesema Dua imelenga kumuombea Mhe. Mchengerwa kwasababu ameleta maendeleo, amani na utulivu ndani ya Rufiji.
"Ametuletea maendeleo na ametutengenezea amani, sasa hivi wafugaji wapo sehemu yao na sisi tupo sehemu yetu hivyo maisha mazuri yanaendelea" amesema Rwanda.
Kiongozi wa Al Qadiri ya Wilaya ya Rufiji, Yusufu Kinjogo amempongeza Waziri Mchengerwa kwa namna alivyoiletea Rufiji maendeleo ambayo yameleta mabadiliko ya kifikra kwa wananchi.
"Tunamshukuru kwa kuibadilisha Rufiji, Rufiji ya leo imebadilika kwani mitaa yote imewekwa lami, Mungu ampe afya njema ili aendelee kuwatumikia wananchi," amesema Kinjojo.
Kwa upande wake, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI Mhe. Mohamed Mchengerwa amewashukuru wote waliandaa Dua hiyo ya kumuombea, kuwaombea Viongozi waliotangulia mbele za haki, kuliombea Taifa pamoja na viongozi wa Serikali ambao wanaongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.
"Nawashukuru sana wazee wa Rufiji, leo tumewakumbuka wazee wetu waliotangulia mbele za haki, tumemkumbuka Mtume wetu Mohamed (S.A.W), tumemuombea Mhe. Rais na viongozi aliowateua katika nafasi mbalimbali na tumeiombea Rufiji ili iendelee kupata maendeleo," Amesema Mhe. Mchengerwa.

Tamisemi yazielekeza halmashauri zenye uwezo kuajiri watumishi wa mikataba
Na. James K. Mwanamyoto OR-TAMISEMI
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais-TAMISEMI (Afya) Dkt. Festo Dugange, amezitaka halmashauri zenye uwezo wa kiuchumi kuajiri watumishi wa mikataba ili kutatua changamoto ya upungufu wa watumishi katika Mamlaka za Serikali za Mitaa
Dkt. Dugange ametoa maelekezo hayo kwa wakurugenzi wa halmashauri nchini, wakati akifunga mkutano wa 15 wa Taasisi ya Maboresho ya Mamlaka za Serikali za Mitaa (TOA) uliofanyika kwa siku mbili katika Ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma uliopo kwenye Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma.
“Ofisi ya Rais-TAMISEMI ilitoa mwongozo maalum wa namna ya kuajiri watumishi wa mikataba na hususani wa sekta ya elimu na afya, hivyo Makatibu Tawala wa Mikoa kawasimamieni Wakurugenzi wa Halmashauri kutekeleza mwongozo huo,” Dkt. Dugange amesisitiza.
Dkt. Dugange amesema, Serikali imeleta fedha nyingi katika halmashauri ambazo zimejenga zahanati, vituo vya afya, hospitali za wilaya na shule na inaendelea kuajiri kwa awamu, hivyo halmashauri zinazokusanya mapato ya kutosha zinapaswa kuajiri watumishi wa mikataba ili waweze kutoa huduma kwa wananchi kupitia mbiundombinu hiyo iliyojengwa na Serikali.
Aidha, Dkt. Dugange amehimiza kuwa, siku zote Ofisi ya Rais-TAMISEMI inaamini watumishi wote waliochini ya TAMISEMI wakifanya kazi kwa bidii na ufanisi, ni dhahiri kwamba kiwango cha utendaji kazi wa Serikali kitakuwa ni zaidi ya asilimia tisini kwani majukumu yanayotekezlezwa na TAMISEMI yanawagusa wa Tanzania wengi.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Tawala za Mikoa wa Ofisi ya Rais-TAMISEMI Bi. Beatrice Kimoleta amesema kuwa, TAMISEMI itaendelea kushirikiana na Taasisi ya Maboresho ya Mamlaka za Serikali za Mitaa (TOA) ili iweze kuwa imara na kutekeleza majukumu yake kikamilifu.

Tamisemi yakusanya tril.1.11/-
OR-TAMISEMI
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa amesema hadi Machi, 2025 Sh.Trilioni 1.11 zimekusanywa sawa na asilimia 93.15 ya lengo la kukusanya Sh.Trilioni 1.60 kwa Mwaka 2024/25.
Akiwasilisha bungeni makadirio ya mapato na matumizi ya Ofisi hiyo kwa Mwaka 2025/26, Waziri Mchengerwa amesema kati ya fedha hizo Sh.Tilioni 61.21 ni kodi ya majengo, Sh. Trilioni 1.04 ni mapato ya ndani ya mamlaka za serikali za mitaa.
Pia, amesema Sh.Bilioni 16.23 ni mapato ya ndani ya taasisi na Sh.Milioni 201.60 ni maduhuli ya mikoa.
Amefafanua kuwa makusanyo hayo yalitokana na ada za wanachuo, tozo, ukusanyaji wa madeni, mauzo ya bidhaa mbalimbali na ushuru unaotozwa na mamlaka za serikali za mitaa kulingana na Sheria ya Fedha za Serikali za Mitaa, Sura 290.
Mh.Mchengerwa amesema kwa kipindi hicho TAMISEMI ilipanga kutumia Sh.Bilioni 541.27 za mapato ya ndani ya halmashauri kwa ajili ya kuchangia utekelezaji wa shughuli za maendeleo. Hadi Machi, 2025 Sh.Bilioni 312.30 sawa na asilimia 57.70 zimetolewa.
Ameeleza kuwa baadhi ya miradi iliyotekelezwa kwa kipindi hicho ni ujenzi wa miundombinu ya elimu, afya, ujenzi wa barabara, machinjio, minada nyumba za walimu na watumishi wa afya, hospitali, vituo vya afya, zahanati, vituo vya polisi, ununuzi wa magreda

Mhe. mchengerwa atoa maagizo mahususi kwa marc na maded
OR TAMISEMI
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Tamisemi Mhe. Mohamed Omary Mchengerwa amewaelekeza Wakuu wote wa mikoa kuwasimiamia Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa kuzingatia vipaumbele vya mwaka 2025/26 kikamilifu.
Waziri Mchengerwa ametoa maelekezo hayo leo Aprili 16, 2025 wakati akiwasilisha bungeni makadirio ya mapato na matumizi ya wizara na taasisi zake kwa mwaka 2025/26.
Amesema vipaombele vya kuzingatia ni kuhakikisha ukusanyaji wa mapato unafikia malengo na kukamilisha ujenzi wa miundombinu ya afya ya msingi, elimu ya msingi na sekondari kulingana na mipango iliyowekwa.
Mhe. Mchengerwa amewaataka kuzingatia kusimamia utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Uchumi wa Kidigitali ikiwemo uwekaji na matumizi ya mifumo na miundombinu ya TEHAMA katika mikoa na mamlaka za serikali za mitaa ikiwa ni pamoja na vituo vya huduma za afya na elimu.
Vilevile amewaagiza kuhakikisha mapato katika mikoa na mamlaka za serikali za mitaa yanakusanywa kupitia mifumo ya TEHAMA ya Serikali pamoja na kufanya ufuatiliaji wa karibu wa mifumo hiyo ili kudhibiti mianya ya upotevu wa mapato.
Aidha, Mhe. Mchengerwa amesema Mikoa na mamlaka za serikali za mitaa kuhakikisha inatekeleza Mikakati ya Uchumi wa Buluu, nishati safi ya kupikia na mabadiliko ya tabianchi na utunzaji wa mazingira.
Ameiagiza mikoa na mamlaka za serikali za mitaa kuendelea kuimarisha mifumo stahimilivu na endelevu ya utoaji wa huduma bora za afya, ustawi wa jamii na lishe ili kuboresha huduma ambayo ni nguzo muhimu katika kufanikisha utekelezaji wa Mpango wa Bima ya Afya kwa Wote
Pia, amewataka wakuu wa mikoa na wakurugenzi kuhakikisha watoto walio chini ya miaka mitano wanajiunga kwenye vituo vya jamii vya kulelea watoto wadogo mchana.
“Kila halmashauri itapimwa utekelezaji wa vipaumbele hivi kwa kuzingatia miradi iliyotengewa bajeti kwa Mwaka 2025/26.

Tamisemi yaomba trilioni 11.78 bajeti 2025/2026
OR-TAMISEMI
OFISI ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) imewasilisha bungeni makadirio ya mapato kwa mwaka 2025/26 yenye takribani Shilingi trilioni 11. 783 kwa ajili ya wizara na taasisi zilizo chini yake.
Bajeti hiyo imeongezeka kutoka Shilingi trilioni 10.125 zilizotengwa mwaka 2024/25 hadi kufikia Shilingi trilioni 11.783 na kuwa na ongezeko la zaidi ya Sh trilioni 1.66.
Akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mohamed Mchengerwa iamesema Shilingi trilioni 3.95 zinaombwa kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo ambapo kati ya fedha hizo Shilingi trilioni 2.5 ni fedha za ndani, ikijumuisha Shilingi bilioni 613.44 za mapato ya ndani ya halmashauri na Shilingi trilioni 1.45 ni fedha za nje.
Pia amesema Shilingi trilioni 7.84 ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida yanayojumuisha mishahara Shilingi trilioni 6.3 na matumizi mengineyo Shilingi trilioni 1.53 ikijumuisha Shilingi trilioni 1. 067 za mapato ya ndani ya halmashauri.
“Tumewasilisha si tu makadirio ya mapato na matumizi, bali tumeweka mbele yetu dira ya matumaini, ramani ya maendeleo na ahadi ya uongozi unaowajibika. TAMISEMI haitafuti sifa ya kisiasa, tunatafuta suluhisho sahihi kwa maisha ya mtanzania wa kawaida.”
Aidha, Mchengerwa ametoa wito kwa mikoa, mamlaka za serikali za mitaa na wananchi wote kushirikiana, kusonga mbele kwa mshikamano.
“Kwa dhamira hii, na kwa imani kubwa katika maono ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tunawasilisha bajeti hii kama zana ya kazi, dira ya matumaini na silaha ya mapinduzi ya kiutawala, kiuchumi na kijamii.”
“Kwa hiyo, tunasema kwa ujasiri mkubwa, TAMISEMI, ndiyo msingi wa maendeleo endelevu. Kila Shilingi ina Jukumu, Kila Kiongozi ana Wajibu na Kila Mwananchi ana Nafasi!”

Tamisemi yapongezwa na benki ya dunia kwa utekelezaji mzuri ujenzi wa miundombinu kupitia mradi wa sequip
Na OR TAMISEMI
Benki ya Dunia imeipongeza Serikali ya Tanzania kupitia Ofisi ya Rais – TAMISEMI kwa ujenzi wa shule mpya zilizojengwa kupitia mradi wa kuboresha Elimu ya Sekondari SEQUIP ambao umepunguza umbali kwa wanafunzi kufuata elimu suala ambalo lilikuwa likiwakatisha masomo yao hasa jinsia ya kike.
Pongezi hizo zimetolewa na Huma Kidwai Mtaalamu wa Elimu kutoka Benki ya Dunia ambaye ni Mtaratibu wa Mradi wa SEQUIP kwa niaba ya Benki ya Dunia baada ya kutembelea shule ya Sekondari ya Amali ya Katerero iliyoko katika Halmashauri ya Bukoba ambayo imejengwa kupitia mradi huo katika Mkoa wa Kagera.
Akisistiza umahiri wa wanafunzi katika shule hizo mpya, Kidwai amewashauri Wakuu wa shule hizo kujifunza mbinu mpya kwa shule Kongwe na kuwa wabunifu ili kuzalisha wanafunzi bora na mahiri.
Akizungumza kwa niaba ya Ofisi ya Rais – TAMISEMI Mratibu wa Mradi wa SEQUIP Richard Makota amesema shule hizo zilizojengwa zinalenga kuwasaidia wanafunzi kupata elimu kwa vitendo na nadharia kutokana na miundombinu iliyowekwa hasa kwa masomo ya Sayansi.
Aidha, Ferdinand Eladius Mkuu wa shule ya Sekondari ya Amali ya Katerero akizungumza kwa niaba ya walimu wenzake amesema uwepo wa shule hiyo umewasaidia wanafunzi kupenda masomo kutokana na upekee wa miundombinu iliyopo

Majaliwa: toa iwe sehemu ya mabadiliko chanya kwenye serikali za mitaa
OR - TAMISEMI
Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa ameeleza uimarishaji wa Taasisi ya Maboresho ya Mamlaka za Serikali za Mitaa(TOA) ili iwe na nguvu na iweze kuishauri Serikali ipasavyo.
Majaliwa ametoa maagizo hayo leo Aprili 14, 2025 wakati akifungua mkutano wa 15 wa TOA unafanyika katika Ukumbi wa Jiji mkoani Dodoma.
Amesema viongozi wa Kitaifa wanaitaka taasisi hiyo kuwa sehemu ya mabadiliko chanya ya mwelekeo wa utendaji ili ichagize maboresho katika Serikali za Mitaa.
”Endeleeni kuhimiza wanachama kufanya kazi kwa weledi na uzalendo ili kuleta matokeo yanayotarajiwa na wananchi.”
“Kwa kuzingatia ukaribu na ushirikiano wenu na wananchi, naamini mnazitambua changamoto zinazowakabili na mnaelewa afua ambazo zikitekelezwa zitawaletea maendeleo. "
Aidha, Mhe. Majaliwa amesema Serikali imesimamia matumizi ya mifumo ya kieletroniki ili kuimarisha ufanisi, uwazi na uwajibikaji katika Mamlaka za Serikali za Mitaa.
Mifumo hiyo ni pamoja na Mifumo ya Uhasibu, Mifumo ya ukusanyaji wa mapato, Manunuzi na Malipo.
"Matumizi ya Mifumo yamesaidia kupunguza urasimu, kurahisisha ulipaji wa malipo na kodi mbalimbali za Serikali na kuboresha ukusanyaji wa mapato hadi kufikia ukusanyaji wa zaidi ya shilingi bilioni 900."
Pia ametumia fursa hiyo kuagiza uongozi wa TOA uwajibike kuhamasisha Mamlaka za Serikali za Mitaa kutanua wigo wa mapato ili kuongeza uwezo wa kujitegemea kimapato na kugharamia shughuli mbalimbali za uendeshaji na utoaji wa huduma.
Kwa upande wake, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mohamed Mchengerwa amewataka viongozi wote wa Mikoa na watumishi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa nchini, waendelee kusimamia maadili na uzalendo, mifumo ya ukusanyaji wa mapato pamoja na mifumo mingine yote iliyoanzishwa na Serikali kwenye ngazi zao.
Pia amewahimiza kusimamia kikamilifu matumizi ya fedha za umma pamoja na utoaji wa huduma bora kwa wananchi na kusisitiza kuwa Serikali chini ya uongozi wa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan umekuwa na ufanisi zaidi katika Serikali za Mitaa.
Awali, Mwenyekiti wa Taifa wa Taasisi ya Maboresho ya Serikali za Mitaa Tanzania, Albert Msovela alisema wataendelea kusimamia taasisi hiyo na kuhakikisha wanatekeleza shughuli zote za Serikali kwa weledi na ufanisi mkubwa.

Serikali ya kuendelea kujenga miundombinu ya maji shuleni.
Naibu Waziri ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Dkt. Festo Dugange amesema Serikali ina mikakati ya kuendelea kujenga miundombinu ya maji shuleni katika kila bajeti ya fedha ili kuepuka milipuko ya magonjwa na pamoja na kuhakikisha kuwa Ujenzi wa miundombinu ya vyoo unaojumuisha wa miundombinu ya maji tiririka.
Mhe. Dkt Dugange ameyasema hayo wakati wa akijibu swali Mbunge wa Viiti Maalum Mhe Minza Simon Mjika katika kipindi cha maswali na majibu aliyeuliza “Je, Serikali ina mpango gani kujenga miundombinu ya maji shuleni ili kuepuka milipuko ya magonjwa?” katika Bunge la bajeti linaloendelea Jijini Dodoma.
“shule 5,311 za Sekondari zina vyanzo vya maji vya uhakika ambapo shule zenye maji ya bomba ni 2,960, visima shule 1,217 na wanaovuna maji ya mvua ni shule 1,134. Aidha, shule 20,509 za msingi zina vyanzo vya maji ya uhakika ambapo shule zenye maji ya bomba ni 10,965, visima shule 4,966 na shule zinazovuna maji ya mvua ni 4,578.” Amesisitiza.
Amesema pia, Serikali imetoa maelekezo kwa miradi yote ya ujenzi ya vitio vya afya na ujenzi wa shule mpya utajumuisha miundombinu ya maji inayohusisha kuvuna maji ya mvua, kuunganisha na mifumo ya Mamlaka za Maji na kuchimba visima.

Mchengerwa: zoezi la upandaji miti kuwapima wakuu wa wilaya na wakurugenzi
OR-TAMISEMI
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI Mhe. Mohamed Mchengerwa amesema utekelezaji wa agizo la upandaji wa miti lililotolewa na Makamu wa Rais Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango, ni sehemu kipimo cha utendaji kazi wa Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri na Makatibu Tawala wa Wilaya.
Waziri Mchengerwa amesema hayo, wakati wa hafla ya kutoa tuzo kwa washindi wa shindano la upandaji miti shuleni ilioyofanyika katika shule ya Sekondari Mwambisi Forest iliyopo wilayani Kibaha mkoani Pwani.
Mhe. Mchengerwa amesistiza kuwa, maelekezo ya Makamu wa Rais ni amri hivyo yatakuwa ni sehemu ya kipimo cha utekelezaji wa majukumu ya Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri, Makatibu Tawala wa Wilaya pamoja na wasaidizi wao.
“Kaimu Katibu Mkuu peleka maelekezo yangu haya mahususi kwenye sekretarieti zote za mikoa na mamlaka za serikali za mitaa ili agizo la kupanda miti litekelezwe,” Waziri Mchengerwa amesisitiza.
Aidha, Mhe. Mchengerwa amewapongeza walimu pamoja na wanafunzi wa shule zote tatu ambazo zimeibuka washindi katika shindano la upandaji miti lililoratibiwa na benki ya NMB.
Kwa upande wake, Mwakilishi wa Benki ya NMB ambaye ni Afisa Mkuu wa Fedha Bw. Juma Kimori, ametangaza washindi katika kampeni hiyo ya upandaji wa miti ambapo Shule ya Sekondari Mwambesi Forest imeibuka mshindi wa kwanza, Shule ya Msingi Ibondo imekuwa ya pili na ya tatu ni Shule ya Sekondari Itimbo.
Benki ya NMB imetoa zawadi ya shilingi milioni 50 kwa mshindi wa kwaza, milioni 30 kwa mshindi wa pili na milioni 20 kwa mshindi wa tatu.

Wakandarasi 457 wa ujenzi wa barabara walipwa, wengine 322 kulipwa hivi karibuni
OR-TAMISEMI
Serikali imelipa madeni ya wakandarasi 457 wa ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya barabara waliokuwa wakidai baada ya kutekeleza mikataba yao kwa kiwango kinachostahili malipo.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe. Mohamed Mchengerwa ameyasema hayo jijini Dodoma akifungua semina ya mafunzo elekezi kwa wakandarasi wazawa kuhusu matumizi ya mfumo wa kielektroniki wa 'Samia Infrastructure Portal' unaolenga kuwawezesha kuomba fedha kwa ajili ya kuimarisha mitaji yao katika miradi ya barabara chini ya usimamizi wa Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (TARURA).
Waziri Mchengerwa amesema hadi kufikia Aprili 9, 2025, wakandarasi hao walikuwa tayari wamelipwa, huku malipo ya wakandarasi wengine 322 yakiwa mbioni kukamilika.
“Hadi kufikia Aprili 11, 2025, Wakandarasi hawa 322 watakuwa wamelipwa na TARURA, maelekezo yangu kwenu TARURA ni kuhakikisha fedha ambazo tayari mmepokea zinagawiwa kwa haraka, kwa usawa na bila upendeleo, watu wapewe haki zao."
“Wakandarasi waliopo katika kanda zote nchini wafikirieni kwa usawa kutokana na kiasi tulichokipokea kutoka Wizara ya Fedha. Keshokutwa mnipe taarifa ya mgawanyo wa fedha hizo kama tulivyokubaliana,”amesema.
Kuhusu semina hiyo maalum ya elimu ya bidhaa ya kifedha iliyoandaliwa kwa ajili ya wakandarasi wazawa, watumishi wa TARURA, na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Waziri Mchengerwa amesema ni fursa muhimu kwa pande zote kupata uelewa wa kina juu ya utaratibu wa bidhaa lengwa, majukumu ya kila upande, na namna ya kusimamia mchakato huo kwa uwazi na ufanisi.
Awali, Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Mhe. Zainab Katimba amesema kuanzishwa kwa hatifungani ya miundombinu ya Samia ni utekelezaji wa maelekezo ya Waziri Mchengerwa na ni moja ya alama muhimu atakazoziacha katika ofisi hiyo, ikionesha namna alivyotekeleza kwa vitendo dira ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuwekeza katika miundombinu na kuwawezesha wakandarasi wazawa.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Idara ya Mikopo wa Benki ya CRDB, Xavery Makwi, amesema hatifungani hiyo ya Samia imewezesha kukusanywa zaidi ya Sh. bilioni 300 ambazo zitawasaidia wakandarasi wazawa kutekeleza kandarasi zao kwa uhakika, tofauti na hali ilivyokuwa hapo awali.

Mchengerwa: Wakurugenzi, msiwaondoe Waganga Wafawidhi kwa matakwa yenu
OR-TAMISEMI
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe. Mohamed Mchengerwa, amewaelekeza Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa nchini kuhakikisha kuwa hawaondoi Waganga Wafawidhi wa vituo vya afya ngazi ya msingi kwa maamuzi ya hiari au kwa utashi binafsi. Badala yake wazingatie taratibu rasmi za kiutumishi na kinidhamu kwa mujibu wa miongozo iliyowekwa.
Mhe. Mchengerwa ametoa agizo hilo alipokuwa akihitimisha mkutano wa mwaka wa Waganga Wafawidhi wa vituo vya kutolea huduma za afya ngazi ya msingi, uliofanyika jijini Dodoma kwa muda wa siku mbili ambao umewakutanisha wataalamu wa afya kutoka ngazi mbalimbali kwa ajili ya kujadili fursa, changamoto na masuala ya kitaaluma yenye lengo la kuboresha utoaji wa huduma katika ngazi ya msingi.
Katika hotuba yake, Waziri Mchengerwa amesisitiza:
“Ninawataka Wakurugenzi watumie vigezo vya kupima utendaji au ubora wa kazi za Waganga Wafawidhi wa vituo vya kutolea huduma za afya msingi—yaani Key Performance Indicators (KPI)—na si maamuzi ya mtu mmoja mmoja, nadhani nimeeleweka vizuri,”amesema.
Agizo hilo la Waziri limekuja kufuatia malalamiko kutoka kwa baadhi ya Waganga Wafawidhi waliodai kuwa wamekuwa wakiondolewa kwenye nafasi zao kwa hila, kinyume na sheria, kanuni na miongozo ya utumishi wa umma.

Mkoa wa Iringa washika mkia matumizi ya Mfumo wa GoTHOMIS.
Mkurugenzi wa Idara ya Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Dkt. Rashid Mfaume, amewataka Waganga wafawidhi wa vituo vya kutolea huduma za afya ngazi ya Msingi kuweka mikakati yenye tija kukabiliana na dosari mbalimbali zinazokwamisha vituo vyao katika matumizi ya mifumo inayobuniwa na OR – TAMISEMI kwa lengo la kurahisisha na kuboresha utolewaji wa huduma za afya kwa wananchi.
Dkt. Mfaume ametoa agizo hilo wakati akihoji sababu za baadhi ya mikoa kushika nafasi ya mwisho kwenye matumizi ya mfumo ulioboreshwa wa usimamizi na uendeshaji wa vituo vya kutolea huduma za afya ya ngazi ya msingi wa ukusanyaji wa taarifa na mapato wa GOTHOMIS wakati wa mkutano wa mwaka wa waganga wafawidhi wa vituo vya kutolea huduma za afya ngazi ya msingi, unaonedelea katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma.
Kwa mujibu wa Dkt. Mfaume, licha ya mkutano huo kuwa fursa ya kujadiliana juu ya changamoto, mafanikio na masuala kadha ya kitaaluma juu ya kada hiyo lakini pia mkutano huo unatumika kupima utendaji kazi wa waganga wafawidhi ili kuboresha utendaji kazi wao na kuondoa dosari mbalimbali zinazotatiza utolewaji wa huduma bora kwa wananchi.
Kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa na Mkurugenzi wa idara ya TEHAMA OR – TAMISEMI Bw. Erick Kitali juu ya utendaji kazi wa mikoa kupitia mfumo wa GOTHOMIS mpaka kufikia mwezi Aprili mwaka 2025, mkoa wa Ruvuma, umeibuka kinara ukifuatiwa na Songwe, Mbeya, Kigoma na Singida huku mikoa mitano ya mwisho ikiwa ni Tabora,Pwani, Shinyanga, Njombe na Iringa ikishika Mkia.

TRIL.1.29/- ZIMEWEKEZWA NGAZI YA AFYA YA MSINGI– Mhe. Dkt. Dugange
Na OR - TAMISEMI, Dodoma
Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Mhe. Dkt. Festo Dugange, amesema kuwa katika kipindi cha miaka minne ya uongozi wa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Serikali imewekeza Sh.Trilioni 1.29 kwenye ngazi ya afya ya msingi pekee.
Ametoa kauli hiyo jijini Dodoma kwa niaba ya Waziri wa Nchi-TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa kwenye kilele cha maadhimisho ya Wiki ya Afya ambayo yamefanyika kwa mara ya kwanza nchini Tanzania mwaka huu kwa lengo la kutambua mchango wa sekta ya afya, kuimarisha uelewa wa jamii, na kutathmini maendeleo yaliyopatikana, yakiwa na kauli mbiu “Tulipotoka, Tulipo, Tunapoelekea; Tunajenga Taifa Imara na lenye Afya.”
Dkt. Dugange ameeleza kuwa fedha hizo zimetumika kuboresha miundombinu na vifaa tiba katika vituo vya afya, ikiwa ni pamoja na ununuzi wa mashine za mionzi za kawaida na za kidigitali (Digital X-ray), pamoja na vifaa vya upasuaji vilivyoongezwa katika vituo 21 vya afya nchini.
Vilevile, amesema Serikali imeimarisha mawasiliano na mshikamano kati ya ngazi ya afya ya msingi na rufaa ili kuondoa usumbufu kwa wananchi waliokuwa wakihitaji huduma za kibingwa.
Katika hatua nyingine, Dkt. Dugange ameeleza kuwa katika kipindi hicho hospitali 129 za Halmashauri zimejengwa, pamoja na vituo vya afya 367, majengo ya huduma za dharura 87, ICU 30, mitambo ya hewa tiba (oxygen plant) 21, na nyumba za watumishi 270. Aidha, hospitali kongwe 50 zimekarabatiwa, maboma ya zahanati 980 yamekamilishwa, na magari 560 yamenunuliwa, yakiwemo magari ya wagonjwa 382 na magari ya usimamizi shirikishi 212.
Ameongeza kuwa jitihada hizo zimechangia kupungua kwa vifo vya akinamama wakati wa kujifungua kutoka 556 kwa kila vizazi hai 100,000 miaka mitano iliyopita hadi kufikia 104 mwaka 2024 na kwamba hilo ni zao la uwekezaji mkubwa katika sekta ya afya ya msingi nchini.

Mchengerwa: Rufiji ina ndoto ya kuwa na majengo ya ghorofa hospitali ya Utete
Na OR-TAMISEMI
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa amesema wananchi wa Rufiji wana ndoto ya kuwa na majengo ya ghorofa yatakayoinua viwango vya utoaji huduma za afya katika Hospitali ya Wilaya ya Utete.
Kauli hiyo ameitoa akiwa katika Hospitali hiyo kabla ya kumkaribisha Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Taifa, Ismail Ussi, kuzungumza na wananchi mara baada ya Mwenge wa Uhuru kukagua ukarabati uliofanyika katika hospitali hiyo muhimu kwa wakazi wa Rufiji.
“Kutokana na kasi ya maendeleo inayosukumwa na Mheshimiwa Rais kwa wananchi wa Rufiji, tuna ndoto ya kupata majengo ya ghorofa katika hospitali yetu ya wilaya, na tunayo ardhi ya kutosha kwa ajili ya ujenzi huo,” amesema Mhe. Mchengerwa.
Aidha, amesema kuwa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameridhia kutolewa sh. milioni 850 kwa ajili ya kuongeza majengo katika Hospitali hiyo ya Wilaya, hatua itakayoboresha utoaji wa huduma kwa wananchi na fedha hizo zinatarajiwa kupokelewa ndani ya mwezi huu wa Aprili.
Mhe. Mchengerwa amesisitiza kuwa wananchi wa Rufiji wana matarajio makubwa ya maendeleo, na kwa uongozi wa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Dkt. Samia Suluhu Hassan, anaamini maendeleo hayo yataendelea kushamiri katika maeneo yote ya wilaya hiyo.
Kwa upande wake, Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Taifa, Ismail Ussi, amesema kuwa maendeleo yaliyofanywa Rufiji, hususan ukarabati wa Hospitali ya Wilaya Utete, ni kielelezo tosha cha mafanikio ya Mwenge wa Uhuru ambao unahimiza utekelezaji wa miradi ya maendeleo nchini.
“Sisi wakimbiza Mwenge wa Uhuru Kitaifa tumeridhishwa na ukarabati na maboresho yaliyofanyika hapa Hospitali ya Wilaya ya Utete, na tunasisitiza huduma ziendelee kutolewa kwa wananchi ambao ndio walengwa wakuu wa jitihada hizi,” amesema Ussi.

Viongozi wa Mikoa na Wilaya waagizwa kuhamasisha wananchi kushiriki Mbio za Mwenge
Na OR-TAMISEMI
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa, amewataka Wakuu wa Mikoa na Wilaya kote nchini kuhamasisha ushiriki wa wananchi katika Mbio za Mwenge wa Uhuru za mwaka 2025, ambazo zinalenga kuchochea utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika halmashauri ili kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi na kuleta maendeleo nchini.
Ametoa agizo hilo akiwa katika Shule ya Msingi Ukombozi, Ikwiriri, kabla ya kumkaribisha Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Taifa, Ismail Ussi, kuzungumza na wananchi waliokusanyika kushuhudia uraghabishaji wa falsafa ya Mwenge wa Uhuru uliofanywa na wanafunzi wa shule hiyo.
Mhe. Mchengerwa amesisitiza kuwa atahakikisha wananchi wanashiriki kikamilifu kwenye maeneo yote ambayo Mwenge wa Uhuru utapita kukagua miradi ya maendeleo na kuwaelekeza Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri kuhakikisha wanahamasisha wananchi kwa nguvu zote kushiriki shughuli hizo muhimu.
“Mbio za Mwenge zinahamasisha maendeleo, na ndio maana zinaambatana na uzinduzi wa miradi ya kimkakati ya maendeleo. Ushiriki wa wananchi ni fursa muhimu ya kuwajengea uelewa katika usimamizi na utekelezaji wa miradi hiyo,” amesema Waziri Mchengerwa.
Aidha, Waziri Mchengerwa amemweleza Kiongozi wa Mbio za Mwenge Taifa, kuwa Wilaya ya Rufiji imepiga hatua kubwa katika miradi ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa shule, barabara, masoko, vituo vya afya na zahanati, miradi ambayo baadhi yake itakaguliwa na Mwenge wa Uhuru mwaka huu.
Kwa upande wake, Ismail Ussi amesema kila Mtanzania anapaswa kuienzi falsafa ya Baba wa Taifa, akisisitiza kuwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameendeleza falsafa hiyo kwa kumkabidhi jukumu la kuongoza Mbio za Mwenge wa Uhuru 2025, ambapo miradi ya maendeleo itakaguliwa na kuzinduliwa pale itakapobainika kutekelezwa kwa viwango stahiki.

Serikali yatoa mwezi mmoja kwa wanafunzi wa kidato cha nne 2024 kubadilisha machaguo ya Tahasusi za Kidato cha Tano
Na OR TAMISEMI, Dodoma
SERIKALI kupitia Ofisi ya Rais-TAMISEMI inatoa fursa ya mwezi mmoja kwa wanafunzi waliohitimu Kidato cha Nne mwaka 2024 kubadili tahasusi au kozi itakayomwandaa kuwa na utaalamu stahiki katika maisha yao ya baadaye.
Utaratibu huo umeanza Machi 31 hadi Aprili 30 mwaka huu.
Akizungumza na waandishi wa Habari leo tarehe 02.04.2025 Jijini Dodoma, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa alisema hatua hiyo inatoa fursa kwa wanafunzi kubadilisha machaguo ya Tahasusi za Kidato cha Tano na Vyuo vya Kati na Elimu ya Ufundi kwenye mfumo wa kielektroniki wa uchaguzi wa wanafunzi watakaojiunga na Kidato cha Tano na Vyuo.
“Hatua hii ni maandalizi ya awali ya uchaguzi wa wanafunzi watakaojiunga Kidato cha Tano na Vyuo vya Serikali kwa mwaka 2025.”
Serikali imekuwa ikitoa fursa kwa wahitimu wa Kidato cha Nne kufanya mabadiliko ya machaguo ya Tahasusi (combination) na Kozi mbalimbali walizozichagua kupitia Fomu ya Uchaguzi (Selform.).
Fursa hii huwawezesha wanafunzi kurekebisha machaguo yao kulingana na ufaulu waliopata kwenye matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Nne yaliyotangazwa na Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA).
Mchengerwa alisema Serikali kupitia Ofisi ya Rais-TAMISEMI imekamilisha utaratibu wa awali wa kuingiza kwenye kanzidata taarifa zilizo kwenye fomu za uchaguzi za wanafunzi kama zilivyojazwa na wanafunzi wakiwa shuleni.
“Baada ya wanafunzi kufanya marekebisho yao, kanzidata hiyo ndiyo itakayotumika kuwachagua na kuwapangia nafasi za Kidato cha Tano na Kozi mbalimbali katika Vyuo vya Kati na vya Elimu ya Ufundi kwa kuzingatia sifa za ufaulu na machaguo yao.”
“Ofisi ya Rais – TAMISEMI inatoa fursa kwa wahitimu wa elimu ya sekondari Kidato cha Nne, mwaka 2024 kubadili machaguo yao ili kutoa nafasi zaidi kwa mwanafunzi kusoma tahasusi au kozi itakayomwandaa kuwa na utaalamu stahiki katika maisha yake ya baadaye.”
Mhe. Mchengerwa alisema hatua hiyo pia itatoa fursa zaidi ya wanafunzi kuongeza machaguo na kufanya machaguo mapya ya Tahasusi na Kozi.
“Napenda kuwasihi wazazi na walezi kushauriana kikamilifu na watoto wao na kupata ushauri wa kitaalamu na kabla ya kufanya machaguo sahihi ya tahasusi na kozi kulingana na ufaulu wao.”
Wanafunzi, wazazi na walezi wanakumbushwa kushauriana kikamilifu ikiwa ni pamoja na kupata ushauri wa kitaalam na kitaaluma kabla ya kufanya mabadiliko ya tahasusi au Kozi.
Mchengerwa amewahimiza wahitimu wote wanahimizwa kufanya marekebisho ya machaguo ya tahasusi na kozi kulingana na ufaulu wao, kwa kuingia kwenye Mfumo wa Uchaguzi wa Wanafunzi unaopatikana kupitia kiunganishi cha selform.tamisemi.go.tz.
Akielekeza namna ya wahitimu kuingia kwenye mfumo, Mchengerwa alisema mhitimu anapaswa kuandika jina lake la mwisho, mwaka wa kuzaliwa na alama za ufaulu alioupata kwenye somo atakaloulizwa na mfumo au swali lolote atakaloulizwa.
“Ni matumaini yangu kuwa wahitimu wote watatumia kwa ukamilifu fursa waliyopewa ya kubadilisha tahasusi na kozi kulingana na ufaulu waliopata. Pia wataweza kusoma tahasusi au kozi ambazo wamefaulu vizuri ama wana malengo nazo zaidi.”
Mhe. Mchengerwa alisema baada ya kukamilika kwa utaratibu huo na wanafunzi kupangiwa shule na vyuo, hakutakuwa na fursa ya wazazi na wanafunzi kubadili tahasusi na kozi zao.
“Ninawasisitiza wanafunzi, wazazi na walezi kutumia muda huo vyema ili kuepusha changamoto zinazoweza kujitokeza mara baada ya matokeo ya uchaguzi wa wanafunzi wa kujiunga na Kidato cha Tano na Vyuo kutangazwa.”
“Baada ya matokeo ya kujiunga na Kidato cha Tano na Vyuo kutangazwa, Ofisi haitashughulikhuduma ya kubadilisha tahasusi na zoezi hili ni bure.”

Ukaguzi maalum ufanyike shule ya wasichana ya Mkoa wa Morogoro.
Na OR TAMISEMI Pwani
Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) Mhe. Halima Mdee imeielekeza Ofisi ya mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG) kufanya ukaguzi maalum katika mradi wa ujenzi wa shule ya Sekondari ya Wasichana ya Mkoa mkoa wa Morogoro.
Mhe. Mdee ameyasema hayo mara baada ya ziara ya kukagua miradi miwili ambayo
ni ujenzi wa nyumba za Wakuu wa Idara na mradi wa ujenzi wa shule ya Sekondari Wasichana ya Mkoa wa Morogoro katika Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro vijijini.
“wote tumetembelea ujenzi wa shule tumeshuhudia Kazi nyingi sana hazijakamilika Kwa kiwango ambacho fedha zimetolewa, Kamati ya Bunge inafanya kazi na Mkaguzi Mkuu wa Serikali kama jicho letu uje ufanye ukaguzi Maalum katika mradi huu” amesisitiza.
Amesema hali ya miundombinu iliyojengwa katika mradi huo hauendani na thamani ya fedha ambayo Serikali imekwishatoa katika mradi huo.
Aidha, Kamati imemuelekeza Afisa Masuuli kuwasilisha Kwa Mkaguzi Mkuu wa Serikali Taarifa ya kina inayohusu matumizi ya fedha zote za mradi huo.
Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI Bw. Atupele Mwambene amesema Ofisi ya Rais TAMISEMI imechukua maelekezo yote yaliyotolewa na Kamati hiyo na kwenda kuyasimamia katika utekelezaji.

Mchengerwa: sitaki kusikia changamoto ya dawa hospitali ya utete
Na OR-TAMISEMI
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa, amesema hataki kusikia tena kuhusu changamoto ya upatikanaji wa dawa katika Hospitali ya Utete na kumtaka Mganga Mkuu wa Wilaya ya Rufiji, Hamis Abdallah, kuhakikisha anashughulikia tatizo hilo ili wananchi waendelee kupata huduma bora.
Mhe. Mchengerwa ametoa maelekezo hayo kwa Mganga Mkuu wa Wilaya, wakati wa ziara yake ya kikazi ya kuhimiza uwajibikaji katika Hospitali ya Wilaya ya Rufiji, iliyopo Utete.
"Mganga Mkuu, umepata nafasi ya kuja Rufiji, hivyo unapaswa kushirikiana na wasaidizi wako kutatua changamoto ya kutopatikana kwa dawa katika eneo hili, ambalo mimi ni Waziri wa TAMISEMI," Mhe. Mchengerwa amesisitiza.
Waziri Mchengerwa ameeleza kuwa, Rufiji haijawahi kukutana na changamoto hiyo ya ukosefu wa dawa na kutolea mfano kipindi alichokuwepo Dkt. Makenge, ambaye aliwahi kuwa Mganga Mkuu wa Wilaya ya Rufiji.
"Mganga Mkuu, suala hili halifurahishi. Sitaki wananchi walalamike tena kuhusu kukosa dawa. Jipange kuhakikisha kuwa dawa hazipungui, na nitafanya uchunguzi ili kubaini tatizo ni nini, kwani Serikali haina tatizo la fedha za madawa," ameongeza Mhe. Mchengerwa.
Aidha, Mhe. Mchengerwa amewapongeza Waganga Wakuu na watumishi wa kada ya afya kwa juhudi zao katika kupunguza vifo vya mama na mtoto na kudhibiti vitendo vya rushwa, hususan dhidi ya akina mama wanaofuata huduma ya afya ya uzazi katika hospitali na vituo vya afya nchini.
Naye, Mmoja wa wananchi wa Wilaya ya Rufiji, Mwema Said, ametoa shukrani kwa Waziri Mchengerwa kwa kuboresha miundombinu katika Hospitali hiyo ambayo kwasasa wananchi kufurahiya wodi zilizojengwa, vifaa tiba vilivyonunuliwa, pamoja na huduma bora zinazotolewa.

Mchengerwa: Serikali imedhamiria kuboresha maisha ya Walimu nchini
Na OR-TAMISEMI
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa, amesema kuwa Serikali ya Awamu ya Sita imejidhatiti katika kuboresha maisha ya walimu nchini, hususan katika maeneo ya maslahi na mazingira ya kazi.
Mhe. Mchengerwa ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na viongozi pamoja na wajumbe wa mkutano mkuu wa Chama cha Walimu Wilaya ya Rufiji, mara baada ya walimu hao kufanya uchaguzi wa viongozi katika Ukumbi wa Chuo cha Maendeleo Ikwiriri.
"Tumedhamiria kuboresha maisha yenu. Binafsi, tangu nikiwa Waziri wa UTUMISHI hadi sasa nikiwa Waziri wa TAMISEMI, nimekuwa mstari wa mbele kupigania madaraja yenu na maslahi ya walimu kwa ujumla," amesisitiza.
Aidha, Waziri Mchengerwa amebainisha kuwa Taifa lina bahati ya kuwa na Rais anayewajali na kuwathamini walimu na kwamba baada ya kupokea ombi la kuwapandisha madaraja walimu, Rais hakusita kulitekeleza, licha ya ukweli kuwa hatua hiyo ilisababisha ongezeko katika bajeti ya mishahara.
Kwa upande wake, Katibu wa Chama cha Walimu Mkoa wa Pwani, Susan Shesha, amemshukuru Waziri Mchengerwa kwa juhudi zake za kupigania maslahi ya walimu tangu akiwa Waziri wa UTUMISHI na kueleza kuwa katika nafasi yake ya sasa kama Waziri wa TAMISEMI, ameendelea kutoa kipaumbele kwa walimu kwa kusimamia miradi ya elimu kwa uadilifu, ili kuhakikisha kuwa inawanufaisha wananchi kwa ujumla.

Laac yaagiza ujenzi wa hospitali ya mji ifakara ukamilike
Na OR-TAMISEMI, Ifakara
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), imeielekeza Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Ifakara kuhakikisha ujenzi wa hospitali ya mji huo unakamilika kwa wakati ili wananchi wapate huduma bora za afya.
Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Halima Mdee, ametoa maelekezo hayo baada ya kutembelea na kukagua miradi miwili ya maendeleo ambayo ni ujenzi wa jengo la utawala na ujenzi wa hospitali ya Mji wa Ifakara.
"Afisa Masuuli aondoe dosari zote zilizobainishwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ili mradi huu ukamilike na kutoa huduma kamili kwa wananchi. Aidha, taarifa ya kila robo mwaka ya maendeleo ya ujenzi huu iwasilishwe kwa CAG kwa ajili ya uhakiki," amesisitiza Mhe. Mdee.
Pia, amemtaka Afisa Masuuli kuhakikisha kuwa zaidi ya Sh. milioni 133, ambazo zilichukuliwa kutoka kwenye fedha zilizotolewa na Serikali Kuu kwa ajili ya ujenzi wa hospitali hiyo, zinarudishwa ili kuendeleza mradi huo.
Vilevile, Mhe. Mdee ameelekeza kuwa utekelezaji wa miradi katika halmashauri hiyo uzingatie sheria, kanuni, na miongozo inayotolewa na Ofisi ya Rais – TAMISEMI.
Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Atupele Mwambene, amesema kuwa ofisi yake imepokea maelekezo hayo na itahakikisha yanatekelezwa kikamilifu kwa usimamizi wa Halmashauri ya Mji wa Ifakara.

LAAC yataka Utekelezaji wa miradi uzingatie Miongozo na Kanuni
OR-TAMISEMI
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), imeielekeza Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mlimba kuhakikisha inazingatia miongozo na kanuni katika utekelezaji wa miradi.
Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Halima Mdee ametoa maelekezo hayo baada ya ukaguzi wa miradi miwili ambayo ni nyumba ya Mkurugenzi wa Halmashauri na kukagua mradi wa wodi tatu (wanaume, wanawake, na watoto) katika hospitali ya Halmashauri.
“Ofisa Masuhuri ahakikishe miradi yote inayotekelezwa inafuata miongozo, sheria, na kanuni zinazotolewa na Ofisi ya Rais – TAMISEMI,” amesisitiza.
Amesema kamati imeongeza kuwa matumizi sahihi ya miongozo, sheria, na kanuni ni muhimu katika kuhakikisha miradi inatekelezwa kwa kuzingatia thamani ya fedha na kuepusha matumizi mabaya ya rasilimali.
Naye, Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Mhe. Dkt. Festo Dugange, amesema kuwa ofisi yake imepokea maelekezo hayo na tayari imeanza kuyafanyia kazi kwa utekelezaji.

Wauguzi imarisheni Usimamizi wa utoaji wa huduma bora za afya nchini - Dkt Dugange
Na OR-TAMISEMI, Dodoma
Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Dkt. Festo Dugange amewaelekeza Wauguzi Viongozi wa ngazi zote za afya nchini kuhakikisha wanaimarisha usimamizi wa utoaji wa huduma bora ili wananchi wote wapate huduma bora na kwa usawa
Dkt. Dugange ameyasema hayo leo Machi 27, 2025 wakati akifungua mkutano Mkuu wa Mwaka wa wauguzi viongozi uliofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa PSSSF Jijini Dodoma wenye kauli mbiu ya inayosema HUDUMA BORA WAJIBU WANGU.
Amefafanua kuwa Serikali ya Awamu ya sita imefanya uwekezaji mkubwa katika sekta ya afya hivyo bila ya kuwepo kwa huduma nzuri na bora kutoka kwa watoa huduma za afya, na hasa Wauguzi, uwekezaji huu hautakua na manufaa.
“Serikali imefanya uwekezaji mkubwa kwenye sekta ya afya ikiwemo ujenzi wa miundombinu ya afya, ununuzi wa vifaa na vifaa tiba, uboreshaji wa mazingira ya kazi, hivyo mapaswa kuwasimamia waliopo chini yenu ili wafanye kazi kwa weledi na uadilifu,” Dkt. Dungange amesisitiza.
Dkt. Dugange amewataka wauguzi wote nchini kuhakikisha wanafanyakazi kwa kuzingatia Sheria, Kanuni, Taratibu, Miongozo na Miiko ya taaluma ili kuepuka malalamiko yasiyokuwa ya lazima katika eneo la utoaji wa huduma za afya msingi nchini.
“Tunatambua kuwa wauguzi wanafanya kazi nzuri sana japo kuna baadhi yenu wachache wanaharibu sifa nzuri ya wauguzi kwa kufanya makosa mbalimbali yanayoweza kuepukwa hivyo msisite kuchukua hatua za kisheria na kinidhamu dhidi ya wote watakaobainika kwenda kinyume, kukiuka maadili ya kitaaluma na kufanya ubadhirifu wa mali za umma, amesisitiza Dkt.Dugange
Aidha, amewataka wauguzi hao kujiendeleza ili kupata wauguzi wenye ujuzi na maarifa zaidi ikiwa ni pamoja na Wauguzi Bingwa watakaosaidia kuimarisha upatikaji wa huduma za kibingwa katika hospitali zetu nchini.

Mchengerwa: daraja la muhoro ni mkombozi kwa wananchi rufiji
Na OR-TAMISEMI
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa, amesema ujenzi wa Daraja la Muhoro utaleta ukombozi kwa wananchi wa Kata ya Muhoro, ambao kwa muda mrefu wamekumbwa na changamoto za usafiri na hata kupoteza maisha wanapovuka Mto Rufiji.
Akizungumza wakati wa ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi huo, Mhe. Mchengerwa amemshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kufanikisha mradi huo wa kisasa wenye thamani ya zaidi ya Sh.Bilioni 17.
“Nimeridhishwa na kasi ya ujenzi, lakini nataka mkandarasi aongeze juhudi ili daraja likamilike ifikapo Julai 2025,” amesisitiza Waziri Mchengerwa.
Kwa mujibu wa Meneja wa Wakala qa Barabara Mijini na Vijijiji (TARURA) Mkoa wa Pwani, Mhandisi Leopold Runji, ujenzi umefikia asilimia 40, tayari nguzo nne kati ya sita zimekamilika na lina urefu wa mita tisa, hivyo litasaidia kuzuia mafuriko.
Nao, Wakazi wa Muhoro, Pili Lwambo na Mikidadi Omary, wameeleza furaha yao, wakisema daraja hilo litaepusha vifo vinavyosababishwa na mamba, kusaidia kina mama kujifungua hospitalini, na kurahisisha usafiri wa watoto kwenda shule.

Mchengerwa atoa miezi miwili barabara za TARURA Ikwiriri zikamilike
Na OR-TAMISEMI, Pwani
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa, amemtaka Meneja wa Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini (TARURA) Mkoa wa Pwani, Mhandisi Leopold Runji, kuhakikisha wakandarasi wanakamilisha ujenzi wa barabara za lami Ikwiriri ndani ya miezi miwili ili wananchi wanufaike na maboresho ya miundombinu hiyo yanayofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita.
Mhe. Mchengerwa ametoa maelekezo hayo wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa barabara hizo wilayani Rufiji.
"Natoa miezi miwili tu, barabara ziwe zimekamilika ifikapo Mei 30, 2025, ikiwa ni pamoja na mitaro na taa za barabarani. Hakutakuwa na nyongeza ya muda," amesisitiza Waziri Mchengerwa.
Ameagiza Meneja wa TARURA kuwasimamia wakandarasi wafanye kazi usiku na mchana, akibainisha kuwa barabara hizo zilipaswa kukamilika Desemba 2024 na iwapo hazitakamilika kwa muda uliopangwa, atamuwajibisha meneja huyo.
Nao, Baadhi ya wananchi, akiwamo Dereva wa bodaboda Ramadhan Mwipi na Mama Lishe Mariam Hamza, wamemshukuru Waziri Mchengerwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuboresha barabara hiyo, wakieleza kuwa imeleta ahueni kubwa kwa usafiri na biashara zao.

LAAC yataka hatua dhidi ya watumishi wazembe Mbeya zichukuliwe
Na OR-TAMISEMI, Mbeya
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), chini ya Mwenyekiti wake Mhe. Halima Mdee, imeielekeza Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya kuchukua hatua dhidi ya watumishi wanaokwamisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo.
Maelekezo hayo yametolewa katika kikao cha majumuisho baada ya ziara ya siku tatu ya ukaguzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa mkoani humo.
"Ofisi ya Mkuu wa Mkoa ichukue hatua za kinidhamu kwa watumishi wote watakaobainika kukwamisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo," amesisitiza
Aidha, Kamati imeitaka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kuongeza kasi ya ufuatiliaji wa miradi yote ya maendeleo, ikiwemo kubaini changamoto zinapojitokeza mapema ili kuepusha athari katika utekelezaji wake.
Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Atupele Mwambene, amesema kuwa Ofisi ya Rais – TAMISEMI imechukua maelekezo hayo na itayafanyia kazi kwa kuhakikisha utekelezaji wake unafuatiliwa ipasavyo.
Kamati hiyo imetembelea na kukagua miradi katika Halmashauri ya Wilaya ya Kyela, Halmashauri ya Wilaya ya Chunya, na Halmashauri ya Wilaya ya Mbalizi, mkoani Mbeya.

“Marufuku malori kupita barabara za Mwendokasi” Mhe. Mchengerwa
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Mohamed Mchengerwa leo Machi 21, 2025 amekemea uharibifu wa barabara unaofanywa na Magari Makubwa (Malori) kupita Mwendokasi huku akizitaka Halmashauri na Wakala ya Barabara Vijijini na Mijini (TARURA) kufikiri namna bora ya kumaliza foleni ndani ya Dar es Salaam.
Mhe. Mchengerwa ameyasema hayo wakati wa hafla fupi ya Utiaji Saini wa Zabuni 9 zilizobeba thamani ya Shilingi Bilioni 221.8 zinazojumuisha Barabara zenye urefu wa Kilomita 84.4 zinazotarajiwa kwenda kuboreshwa katika Halmashauri za Dar es Salaam chini ya Mradi wa Uendelezaji wa Jiji la Dar es Salaam Awamu ya Pili (DMDP TWO).
Akizungumza wakati wa Hotuba yake Mhe. Mchengerwa amesema Mhe. Rais hatamani kuona foleni, Halmashauri kaeni fikirini namna ya kumaliza foleni ndani ya Jiji hili, mmetoa Kibali Magari kupita Mwendokasi afadhali kwa Magari madogo lakini sasa yanapita mpaka malori, barabara zimeanza kuharibika. Malori kuanzia sasa nisisikie yamekatisha ndani ya barabara za Mwendokasi.
Lakini pia tutakwenda kufanya mapitio hii asilimia ya makusanyo ya mapato ya ndani inayopaswa kwenda kwenye barabara isiwe 10% ili muifanye TARURA iwe na uwezo wa kufanya kazi masaa 24 kusimamia ujenzi wa barabara katika maeneo yetu.
Nendeni mkafungue barabara ambazo watu wanapaswa kupita kumaliza foleni, TARURA mkoa nendeni mkafikiri nini kifanyike ili mtengeneze barabara za kimkakati zinazoweza kupunguza foleni".
Mhe. Mchengerwa ameshuhudia Utiaji Saini wa Mikataba ya Ujenzi wa Barabara kupitia DMDP zenye urefu wa Km. 84.4.

Mhe. Mchengerwa Utiaji saini wa Mikataba ya ujenzi wa barabara km. 84 za Dar es salaam
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Mohamed Mchengerwa leo Machi 21, 2025 ameshuhudia Utiaji Saini wa Zabuni 9 zilizobeba thamani ya Shilingi Bilioni 221.8 zinazojumuisha Barabara zenye urefu wa Kilomita 84.4 zinazotarajiwa kujengwa katika Halmashauri za Dar es Salaam chini ya Mradi wa Uendelezaji wa Jiji la Dar es Salaam Awamu ya Pili (DMDP II).
Miongoni mwa zabuni Hizo, Zabuni 2 zenye Jumla ya thamani ya Sh.Bil 47.1 ni kwa ajili ya Halmashauri ya Manispaa ya Temeke ambapo Bilioni 25.9 zitakwenda kutengeneza Barabara za Masuliza, Kilimahewa na Tuangoma zenye jumla ya kilomita 10.21 huku Bilioni 21.1 zikielekezwa kwa ajili ya Barabara za Konisaga 1, Konisaga 3, Kurasini, Taningira uhasibu, Kizota, Lushoto, Pendamoyo, Mandera, Mkumba Miburani, Kipati pamoja na Vivuko 6 vya Mdeda, Mpeta, Baajun, Msalaka Mashine ya maji, Shehe muckhi, na Azimio Msalaka.
Akizungumza katika Hafla hiyo Mhe. Mchengerwa amesema Matarajio ya Rais wetu ni kulifanya Jiji la Dsm kuwa Miongoni mwa Majiji ya Kisasa, Jiji shindani (Metropolitan city) na fedha hizi ni za Watanzania, Wakandarasi wanapokabidhiwa Mikataba hii waende kuitendea haki, na Wakandarasi walioshindwa kutimiza Makubaliano naelekeza kutengua Mikataba, taratibu zote zifuatwe bila kuingiza hasara Serikali maana yake ni lazima walipe fedha zote walizopewa na Serikali. Taratibu hizi zianze na ntaanza kuzifatilia kwa katibu mkuu"
"Na Kampuni hizi tulizozipa Kazi leo hii kusaini Mikataba wasipotekeleza makubaliano na kushindwa kutekeleza kwa muda tuliokubaliana taratibu za kuvunja Mkataba zifuatwe na wawe blacklisted wasiruhusiwe kupata Mkataba wowote ndani ya Nchi hii. Kwenye Mikataba hii tuliyosaini leo hatutakuwa na nyongeza hata siku moja". Alisema Mhe. Mchengerwa.
Hafla hiyo imefanyika katika Ukumbi wa Mradi (Millenium Tower) na kuhudhuriwa na Viongozi mbalimbali.

Mhe. Mdee: Wajibu wenu ni kuhudumia wananchi kwa ufasaha
Na OR-TAMISEMI, Mbeya
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), Mhe. Halima Mdee, amewataka Watumishi wa Umma na Viongozi kutekeleza wajibu wao kwa ufasaha ili kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi.
Mhe. Mdee akizungumza katika ziara ya Kamati hiyo kukagua miradi mbalimbali ya afya na elimu inayotekelezwa Halmashauri ya Kyela, mkoani Mbeya, amesema "Kila mmoja atekeleze wajibu wake kwa wakati na kwa ufasaha, viongozi hawatakuwa na haja ya kuja kukagua."
Ameeleza kuwa kutokana na ukubwa wa nchi, haiwezekani kwa kiongozi mmoja kutembelea kila mahali kutoa huduma, hivyo majukumu hayo yamekabidhiwa kwa Watumishi wa Umma ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma stahiki.
Aidha, amewataka Watumishi wa Umma kutekeleza maelekezo yanayotolewa na Kamati ya Kudumu ya Bunge na kuhakikisha wanazitatua dosari zinazobainishwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa kutoa taarifa sahihi.
Naye, Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Mhe. Dkt. Festo Dugange, amesema Ofisi yake imechukua maelekezo yote yaliyotolewa na Kamati na itayasimamia kikamilifu katika utekelezaji wake.
Pia, Mhe. Dkt. Dugange amewataka Watumishi wa Umma kuhakikisha fedha zinazotolewa kwa ajili ya miradi ya maendeleo zinatumika ipasavyo ili miradi hiyo ikamilike kwa wakati na kuzingatia thamani ya fedha.

Mchengerwa: bil.82.84/- zimekopeshwa kwa wanawake,vijana na watu wenye ulemavu
Na OR-TAMISEMI
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe. Mohamed Mchengerwa, amesema katika mwaka wa fedha 2024/25, serikali imetoa mikopo yenye thamani ya Sh. bilioni 82.84 kwa vikundi 8,275 vya wanawake, vijana, na watu wenye ulemavu kupitia mpango wa asilimia 10 ya mapato ya halmashauri.
Waziri Mchengerwa ameeleza hayo wakati akiwasilisha mapitio ya utekelezaji wa bajeti ya mwaka wa fedha 2024/25 na makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka 2025/26 katika vikao vya kamati za kudumu za Bunge linaloendelea jijini Dodoma.
Ameeleza kuwa kati ya fedha hizo Sh. Bilioni 40.71 zimetolewa kwa vikundi 4,557 vya wanawake, Sh.Bilioni 36.64 kwa vikundi 2,827 vya vijana na Sh.Bilioni 5.48 kwa vikundi 891 vya watu wenye ulemavu.
Waziri Mchengerwa amefafanua kuwa
Ofisi ya Rais – TAMISEMI imeandaa mwongozo wa ukomo wa mkopo ambao utawezesha halmashauri kusimamia utoaji wa mikopo yenye tija kwa jamii na kulingana na mwongozo huo kiwango cha juu cha mkopo kwa kikundi ni sh. milioni 150 na kiwango cha chini cha mkopo ni sh.500,000.
Aidha, Waziri Mchengerwa amebainisha kuwa hali ya upatikanaji wa bidhaa za afya kwenye vituo vya kutolea huduma imeimarika ambapo upatikanaji wa dawa umeongezeka kutoka asilimia 63.00 mwaka 2023/24 hadi asilimia 79.30 Januari 2025, ikiwa ni ongezeko la asilimia 16.30.

Kamati ya Bunge yaitaka TAMISEMI kumchunguza Mkandarasi wa mradi wa TACTIC Kahama
Na OR-TAMISEMI, Shinyanga
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya TAMISEMI imeielekeza Ofisi ya Rais - TAMISEMI kupitia upya mkataba wa mkandarasi wa kigeni, Sichuan Road and Bridge Group Corporation, na kuchukua hatua za haraka kutokana na kushindwa kutekeleza kwa wakati mradi wa TACTIC awamu ya kwanza katika Wilaya ya Kahama, Mkoa wa Shinyanga.
Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Justin Nyamoga, ametoa maelekezo hayo wakati wa ziara ya kamati hiyo ya kukagua utekelezaji wa mradi huo wa ujenzi wa barabara za katikati ya mji na mifereji ya maji ya mvua wenye thamani ya sh. bilioni 20.864.
Kwa mujibu wa mkataba, mradi huu ulianza kutekelezwa Novemba 20, 2023, na ulipaswa kukamilika Februari 19, 2025. Hata hivyo, hadi sasa utekelezaji wake uko katika asilimia 48%, hali iliyosababisha kuongezewa muda wa ziada wa miezi mitatu hadi Mei 19, 2025.
Mhe. Nyamoga amesema "Kamati haitatoa maelekezo nini kifanyike, lakini ninyi nendeni mkasome mkataba wake, kaangalieni changamoto anazozisababisha, ikiwemo kuwafilisi Watanzania ambao yeye amechukua vitu kwao na hajawalipa."
Naye, Naibu Waziri wa TAMISEMI, Mhe. Zainab Katimba, akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Mhe. Mohamed Mchengerwa, amesema serikali itasubiri kwa miezi mitatu kuona kama mkandarasi huyo atakamilisha kazi na iwapo atashindwa, serikali itavunja mkataba na mkandarasi huyo hatakuwa na sifa ya kupata kazi nchini.
Kwa upande wake, Mhandisi Rogatus Mativila, Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais – TAMISEMI anayeshughulikia Miundombinu, amesema moja ya changamoto zinazokwamisha miradi mingi ni kuhamisha pesa za miradi kwenda kwenye shughuli nyingine baada ya kuzipokea.
Mradi huu wa Kupendezesha Miji (TACTIC) unatekelezwa katika Halmashauri 45 nchini, ikiwemo Kahama, ambapo awamu ya kwanza inahusisha, Ujenzi wa barabara za katikati ya mji – Kilomita 12.03, Barabara za eneo la viwanda Zongomela – Kilomita 3.06, Ujenzi wa mifereji ya maji ya mvua – Chelsea – Lyazungu na Shunu Magobeko (Kilomita 4.9)

Mchengerwa amtaka Mkandarasi wa daraja la Mbambe kuongeza kasi ya ujenzi
Na. OR-TAMISEMI, Rufiji Pwani
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa, amemtaka mkandarasi wa Kampuni ya Nyanza Road Works kuongeza kasi ya ujenzi wa Daraja la Mbambe lenye urefu wa mita 81 ili likamilike kwa wakati na kuondoa adha inayowakabili wananchi wa Wilaya ya Rufiji.
Mhe. Mchengerwa akitoa maelekezo hayo wakati wa ziara yake ya kikazi katika Kijiji cha Mbambe ya kufuatilia maendeleo ya ujenzi wa daraja hilo, amesema; "Mkandarasi ongeza kasi ya ujenzi wa daraja hili kwani asilimia 22 iliyofikiwa bado ni ndogo sana. Kwa mwendo huu, mvua zikiongezeka zitaleta changamoto itakayokwamisha ujenzi."
Aidha, amewataka wananchi wa Kijiji cha Mbambe kushirikiana na uongozi wa wilaya kwa kutoa taarifa pale wanapoona hali ya kusuasua katika ujenzi wa daraja hilo na kuwahakikishia kuwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan tayari ametoa fedha kwa ajili ya fidia kwa wote waliopitiwa na mradi huo, ambao unahusisha pia ujenzi wa barabara za maingilio zenye urefu wa kilomita 3.
"Mkuu wa Wilaya, naelekeza Meneja wa TANROADS wa mkoa kuhakikisha kuanzia wiki ijayo fidia inalipwa kwa wale wote waliokwishahakikiwa madai yao. Rais Samia ameshatoa shilingi milioni 500 kwa ajili ya fidia," ameagiza Mhe. Mchengerwa.
Hata hivyo, Waziri Mchengerwa amewataka wananchi wa Mbambe na Rufiji kwa ujumla kupuuza taarifa potofu kwamba mradi wa daraja hilo umesimama, akisisitiza kuwa ujenzi unaendelea.
Awali, Msimamizi wa Mradi kutoka Kampuni ya Nyanza Road Works, Mhandisi Emmanurel Owoya, amesema kuwa ujenzi huo umefikia asilimia 22, ambapo tayari nguzo za msingi 64 kati ya 107 zimejengwa na Sh.Bilioni 24.16 zitatumika kukamilisha ujenzi wa Daraja la Mbambe, likijumuisha barabara za maingilio za kilomita 3 kwa pande zote mbili za daraja.

LAAC yaielekeza iringa kukamilisha ujenzi wa uzio wa madarasa ya Awali
Na OR-TAMISEMI, Iringa
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), imeielekeza Halmashauri ya Manispaa ya Iringa Mjini kuhakikisha inakamilisha ujenzi wa uzio katika madarasa ya awali ya Shule ya Msingi Uyole.
Maelekezo hayo yametolewa katika kikao cha majumuisho baada ya Kamati hiyo kufanya ziara ya kukagua miradi ya maendeleo katika Halmashauri hiyo na Mjumbe wa Kamati hiyo ambaye Mbunge wa Kilindi, Mhe. Omary Kigua kwa niaba ya Mwenyekiti wa LAAC, Halima Mdee.
Amesema “Afisa Masuhuri hakikisha uzio katika madarasa ya awali uwe umejengwa kabla ya kukamilika kwa mwaka wa fedha 2025/26, na taarifa ya ujenzi huo iwasilishwe kwa CAG kwa ajili ya mapitio.”
Pia, Amesema Kamati imeelekeza Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo kuhakikisha kuwa ujenzi wa jengo la kufulia katika Kituo cha Afya Itamba unakamilika kabla ya mwisho wa mwaka huu wa fedha.
Naye, Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Mhe. Dkt. Festo Dugange, amesema kuwa serikali kupitia TAMISEMI itafanyia kazi mapungufu yote yaliyoainishwa na Kamati ili kuhakikisha miradi inatekelezwa kwa viwango vinavyokubalika kwa manufaa ya wananchi.
Miradi iliyokaguliwa na kamati hiyo ni pamoja na Ujenzi wa machinjio ya kisasa Ngelewala, Ujenzi wa Shule ya Msingi ya Mkondo Mmoja Uyole na Ujenzi wa Kituo cha Afya Itamba ambapo kamati imesisitiza ikamilike kwa wakati ili kuboresha huduma kwa wananchi wa Iringa.

LAAC yataka dosari zilizobainishwa na CAG Halmashauri ya Wilaya Kilolo zitatuliwe
Na OR-TAMISEMI, Kilolo
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), imeielekeza Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo kuhakikisha inaziondoa dosari zote zilizobainishwa na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) katika ujenzi wa Shule ya Wasichana ya Lugalo, mkoani Iringa.
Maelekezo hayo yametolewa na Mwenyekiti wa kamati, Halima Mdee baada ya kamati kutembelea na kukagua ujenzi wa shule hiyo.
"Dosari zote zilizobainishwa na CAG katika utekelezaji wa mradi huu zinaondolewa na kuhakikisha miundombinu muhimu inakamilika," amesema Mhe. Mdee.
Kamati pia imeelekeza Afisa Masuuli wa Halmashauri kuandaa taarifa yenye maelezo ya kina na mchanganuo wa matumizi ya fedha zote za mradi huo na kuiwasilisha kwa CAG kwa ajili ya uhakiki.
Aidha, kamati imeitaka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kufanya tathmini ya kina na kufuatilia kwa karibu utekelezaji wa mradi huo, huku ikichukua hatua za haraka iwapo kutabainika ukiukwaji wa sheria na taratibu.

Serikali kujenga na kukarabati shule ya msingi Kakoyoyo
Na OR-TAMISEMI, Geita
Serikali imeahidi kuanza ukarabati na ujenzi wa majengo ya Shule ya Msingi Kakoyoyo, ambayo ilifungwa baada ya baadhi ya majengo yake kutitia, kupata nyufa, na kuanguka kufuatia mvua kubwa zilizonyesha mapema 2024 katika Wilaya ya Bukombe, Mkoa wa Geita.
Shule hiyo, iliyojengwa kwa nguvu za wananchi mwaka 1999, ilihudumia wanafunzi 934 ambao kwa sasa wamelazimika kusoma katika Shule ya Msingi Igwamanoni kwa kutembea umbali wa zaidi ya kilomita 13.
Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Mhe. Zainab Katimba, ametembelea shule hiyo na kuthibitisha kuwa serikali itaanza ukarabati mara baada ya tathmini ya wataalamu kukamilika.
“Tumeona uhitaji mkubwa wa kurejesha shule hii, na kupitia mapato ya ndani, serikali kuu, pamoja na wadau wa maendeleo, tutahakikisha ukarabati unafanyika ili wanafunzi waendelee kusoma katika mazingira bora,” amesema.
Naye, Diwani wa Kata ya Bulega, Mhe. Erick Kagoma, ameipongeza serikali kwa hatua hiyo, akieleza kuwa kurejeshwa kwa shule hiyo kutapunguza adha ya wanafunzi kutembea umbali mrefu.
Ziara hiyo imefanyika kufuatia ombi la Mbunge wa Jimbo la Bukombe, Mhe. Dkt. Doto Mashaka Biteko, ambaye pia ni Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, ili kuwapa wananchi taarifa kuhusu hatua za serikali katika kuboresha shule hiyo.

Kamati ya Bunge yaelekeza ujenzi wa shule mpya za Muleba zikamilike ifikapo Aprili, 2025
Na OR-TAMISEMI
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya TAMISEMI imeuagiza uongozi wa Wilaya ya Muleba, Mkoa wa Kagera, kuhakikisha ujenzi wa Shule ya Sekondari Biija na Shule ya Sekondari ya Amali (Ufundi) Mubunda unakamilika ifikapo Aprili 2025 ili wanafunzi waanze masomo.
Miradi hiyo inafadhiliwa na Serikali kwa asilimia 100 kupitia mradi wa SEQUIP, ambapo kila shule imepokea Sh.Milioni 584.2 na ujenzi wake unafanyika kwa njia ya 'Force Account'.
Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Justin Nyamoga, akizungumza katika ziara ya kamati ya kukagua ujenzi huo, amesema Shule ya Biija imejengwa ili kupunguza umbali wa wanafunzi wanaosafiri kutoka maeneo ya mbali na kuagiza pindi ujenzi utakapokamilika, walimu waletwe haraka na wanafunzi waanze masomo bila kuchelewa.
Pia, amesisitiza kuwa wanafunzi wanaotembea mwendo mrefu wahamishiwe katika shule hiyo ili kurahisisha upatikanaji wa elimu.
Kwa upande wake, Naibu Waziri wa TAMISEMI, Mhe. Zainab Katimba, akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Mhe. Mohamed Mchengerwa, amehimiza viongozi wa Halmashauri kuhakikisha mradi unakamilika kwa wakati na miundombinu ya shule inatunzwa ili iweze kuwanufaisha vizazi vingi na kwamba ucheleweshaji wa miradi haukubaliki.
Aidha, Mhe. Katimba amemtaka Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba kuimarisha matumizi ya mfumo wa kielektroniki wa manunuzi ya umma (NEST) ili kuepusha ucheleweshaji wa miradi.

Mchengerwa atoa maelekezo nane mahsusi kwa Mamlaka za Serikali za Mitaa
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa ametoa maelekezo mahsusi nane kwa viongozi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa ikiwamo kufanya tathmini ya kina na kuchukua hatua za haraka kwa watumishi wanaoshiriki kuhujumu mfumo wa mapato kwenye maeneo yao.
Akifunga Machi 12, 2025 Mkutano Mkuu wa 39 wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa (ALAT) jijini Dodoma kwa niaba ya Waziri Mchengerwa, Naibu Waziri wa Ofisi hiyo, Mhe. DFesto Dugange, amewataka wafanye tathmini hiyo ili kuhakikisha hakuna upotevu au uvujaji wa mapato mikononi mwa watumishi.
Aidha, ameelekeza kupatiwa taarifa ya namna kila Halmashauri zilivyokusanya katika vyanzo kodi ya majengo, ushuru wa mabango na kodi ya Ardhi ili ili kupima ufanisi.
Pia, ameagiza Halmashauri zisimamie kikamilifu utoaji wa huduma bora za afya ili kuondoa malalamiko ya wananchi kwa serikali na ziweke mikakati madhubuti ya kudhibiti upotevu wa fedha za uchangiaji wa huduma za afya.
Kuhusu elimu, ameelekeza wahakikishe wanasimamia uandikishaji wa madarasa ya awali, darasa la kwanza na makundi mengine kutokana na hali kutoridhisha kwa baadhi ya mikoa sambamba na kuthibiti mdondoko wa wanafunzi.
Mhe. Waziri Pia ameelekeza Halmashauri zinazotekeleza miradi ya TACTIC ambayo Wakurugenzi wamesaini mikataba, hakikisheni wanasimamia utekelezaji kwa viwango, ukubwa wa kazi, muda unaotakiwa na fedha itumike kama ilivyokusudiwa.
Pamoja na hayo, ameagiza Wakurugenzi kusimamia mikopo ya asilimia 10 na kuondoa changamoto zinazolalamikiwa kwa kuzingatia sheria, kanuni na miongozo iliyoandaliwa kusimamia mikopo hiyo.

Kamati ya Bunge yahimiza maslahi ya watumishi wapya yazingatiwe
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya TAMISEMI imeiomba serikali kuendelea kuboresha maslahi ya watumishi na kuwalipa stahiki zao, hususan kwa watumishi wapya, ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.
Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Justin Lazaro Nyamoga ametoa kauli hiyo wakati wa ziara ya kukagua mradi wa Hospitali Mpya ya Halmashauri ya Wilaya ya Uvinza ambayo ni miongoni mwa hospitali mpya 129 zilizojengwa na serikali kupitia Ofisi ya Rais – TAMISEMI.
"Suala la watumishi katika baadhi ya mikoa, ikiwemo Kigoma, ni changamoto. Kamati inasisitiza mambo mawili: kuongeza watumishi hasa pale fursa zinapojitokeza, na kuhakikisha malipo stahiki yanatolewa kwa watumishi wapya na wanaohama ili kuwapa moyo wa kufanya kazi kwa bidii," amesema Mhe. Nyamoga.
Aidha,Kamati hiyo imetoa maelekezo kwa Ofisi ya Rais – TAMISEMI kuhakikisha jenereta kubwa linapelekwa katika Hospitali ya Wilaya ya Uvinza, kwani lililopo sasa halina uwezo wa kusambaza umeme kwa hospitali nzima.
Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Mhe. Zainab Katimba, akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Mhe. Mohamed Mchengerwa, ameahidi kuyafanyia kazi maelekezo ya kamati huku akiwataka watumishi wa umma kuendelea kutoa huduma bora kwa wananchi.

Mchengerwa: Rais Samia ametoa kipaumbele kwa Serikali za Mitaa kuchochea maendeleo
Na OR-TAMISEMI, Dodoma
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa amesema Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameendelea kuweka mkazo katika kuimarisha serikali za mitaa kama chachu ya maendeleo ya wananchi kwa kuongeza rasilimali, kuboresha mifumo ya utendaji, na kuimarisha uwajibikaji wa viongozi wa halmashauri.
Waziri Mchengerwa amesema hayo Machi 11, 2025 kwenye ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa 39 wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT) uliofanyika jijini Dodoma.
“Maendeleo siyo ahadi, bali ni hatua zinazochukuliwa kila siku kwa vitendo. Tunamshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwa mstari wa mbele kuhakikisha serikali za mitaa zinakuwa msingi wa maendeleo ya wananchi. Serikali yake imeonesha kuwa maendeleo yanaanzia chini kwenda juu, na kwa kuimarisha serikali za mitaa, tumewawezesha wananchi kushiriki moja kwa moja katika mchakato wa maendeleo,” amesema Mhe. Mchengerwa.
Ameeleza kuwa uwekezaji mkubwa umefanyika katika sekta ya elimu, afya, na miundombinu, hatua inayowezesha wananchi kushiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi.
Aidha, Waziri Mchengerwa amewahimiza viongozi wa serikali za mitaa kuwa wabunifu, kuzingatia uadilifu katika utendaji wao, na kushirikiana na serikali kuu ili kuhakikisha maendeleo ya taifa yanapiga hatua kwa kasi zaid

Kamati ya Bunge yavutiwa na ubunifu wa TARURA ujenzi wa daraja la kamba za chuma Mbulu
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya TAMISEMI imepongeza ubunifu wa Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini (TARURA) katika ujenzi wa daraja la kamba za chuma kwenye barabara ya Tipri, Halmashauri ya Mji wa Mbulu, Mkoa wa Manyara ambalo limeondoa kikwazo kikubwa cha shughuli za kiuchumi na kijamii wakati wa msimu wa mvua.
Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Justin Nyamoga, ametoa pongezi hizo katika ziara ya kukagua mradi huo katika mto Mtunguli ambao umegharimu Sh. milioni 158.9 kutoka kwenye tozo ya mafuta.
Mhe. Nyamoga ameshauri TARURA kujenga kingo za daraja hilo ili kuimarisha usalama wa watembea kwa miguu na waendesha pikipiki wanaoweza kuteleza na kuanguka mtoni.
Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mhe. Zainab Katimba, akizungumza kwa niaba ya Waziri wa TAMISEMI Mhe. Mohamed Mchengerwa, amesema daraja hilo la watembea kwa miguu lina uwezo wa kubeba tani 1.5 na litadumu kwa zaidi ya miaka 70 na kutoa wito kwa wananchi kulinda miundombinu hiyo muhimu.
Daraja la Tipri, lililojengwa kwenye bonde la mto Mtunguli, litasaidia zaidi ya wananchi 3,900 waliokuwa wakikwama na kupoteza mawasiliano wakati wa mvua

Maafisa Elimu wahimizwa kuimarisha usimamizi wa elimu nchini
Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Elimu, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Dkt. Emmanuel Shindika, amewataka Maafisa Elimu wa Mikoa na Halmashauri kuhakikisha wanaimarisha ufuatiliaji na usimamizi wa elimu katika maeneo yao ili kuleta mabadiliko chanya kwenye Sekta ya Elimu nchini.
Dkt. Shindika ametoa wito huo leo Machi 7, 2025 alipokuwa akifunga Mkutano Mkuu wa Umoja wa Maafisa Elimu wa Mikoa na Halmashauri (REDEOA), uliofanyika Jijini Dar es Salaam ambao unatathmini utekelezaji wa shughuli za elimu kwa kipindo cha kuanzia mwezi Julai hadi Desemba, 2024.
Amesema ni muhimu kuimarisha usimamizi wa elimu kwa kuhakikisha uandikishaji wa wanafunzi wa shule za awali na msingi unasimamiwa kwa ukaribu ili kufanikisha malengo ya serikali katika Sekta ya Elimu.
"Uandikishaji wa wanafunzi wa awali na msingi bado ni changamoto katika maeneo yenu. Hakikisheni mnasimamia kwa karibu suala hili ili kutimiza malengo yaliyowekwa na Serikali," amesisitiza.
Pia amewataka Maafisa Elimu kusikiliza na kutatua changamoto zinazowakabili walimu ili kuongeza tija na ufanisi katika ufundishaji na kuimarisha mahusiano mazuri kazini, kuwalipa walimu stahiki zao kwa wakati, na kuhakikisha malipo ya likizo hayacheleweshwi.
Aidha, amewaelekeza Viongozi hao kusimamia kwa weledi utekelezaji wa miradi ya elimu katika maeneo yao, ili ikamilike kwa wakati na kuendana na thamani ya fedha iliyotengwa huku akisisitiza ushirikiano wa karibu kati ya Maafisa Elimu na Wadau mbalimbali wa elimu ili kuimarisha ubora wa elimu nchini.

Kamati ya Bunge ya TAMISEMI yataka ulinzi wa daraja la mawe Garkawe
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya TAMISEMI, imewataka wananchi kuacha shughuli za kilimo kando ya mto ulipojengwa Daraja la Mawe la Garkawe katika barabara ya Maretadu - Garkawe, Wilaya ya Mbulu mkoani Manyara ili kulinda miundombinu ya daraja hilo.
Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Justin Nyamoga ametoa wito huo katika ziara ya kukagua mradi wa daraja hilo, ambalo limejengwa kwa fedha za tozo ya Mafuta kiasi cha Sh.Milioni 470.95.
Aliutaka uongozi wa Wilaya ya Mbulu kufuatilia na kuzungumza na wananchi ili kuhakikisha shughuli za kilimo haziendelei karibu na daraja hilo.
"Madaraja haya yanajengwa kwa gharama kubwa, na tunatambua kuwa wananchi wanahitaji kulima. Hata hivyo, ni muhimu kuacha nafasi ili mto huu usiendelee kupanuka, kwani inaweza kusababisha madhara kwenye daraja," amesema Mhe. Nyamoga.
Kwa upande wake, Naibu Waziri, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Mhe. Zainab Katimba, akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa, amesema kuwa ujenzi wa madaraja ya mawe, ikiwamo la Garkawe, umesaidia kupunguza gharama za ujenzi kutokana na wepesi wa upatikanaji wa malighafi.
"Madaraja haya yaliyotumia teknolojia ya mawe yamejengwa 238 kwa gharama ya jumla ya Sh.Bilioni 12.52 nchini kote. Ni hatua kubwa katika kupunguza gharama za ujenzi na kuongeza ufanisi," amesema Mhe. Katimba.

Ubora wa miundombinu uendane na ubora wa huduma – Dkt. Mfaume
Mkurugenzi wa Idara ya Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii kutoka Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Dkt. Rashid Mfaume, amewataka watumishi wa sekta ya afya kutoa huduma bora zinazoendana na ubora wa miundombinu ambayo serikali imewekeza katika vituo vya kutolea huduma za afya.
Dkt. Mfaume ametoa maelekezo hayo alipofanya ziara katika Hospitali ya Wilaya ya Bahi, ikiwa ni sehemu ya ziara shirikishi ya usimamizi wa upatikanaji wa huduma mbalimbali za Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii katika Mkoa wa Dodoma.
"Tuna majengo mazuri na vifaa vyote vya msingi ambavyo vimetolewa na serikali. Hivyo, ubora wa majengo uendane na huduma zinazotolewa kwa kuzingatia miongozo ya afya," amesema Dkt. Mfaume.
Aidha, amesisitiza kuwa kuna miongozo mbalimbali kutoka Wizara ya Afya na Shirika la Afya Duniani (WHO) inayopaswa kuzingatiwa katika utoaji wa huduma kwa wagonjwa.
Vilevile, amewakumbusha wasimamizi wa miradi ya afya inayoendelea kutekelezwa nchini kuhakikisha kuwa miradi hiyo inazingatia thamani ya fedha ili ikidhi malengo ya serikali ya kuboresha huduma kwa wananchi.

Prof.Mkenda asisitiza umuhimu wa Elimu ya Amali kukuza ujuzi
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Prof. Adolf Mkenda, amesisitiza umuhimu wa elimu ya amali kama njia ya kukuza ujuzi wa kiutendaji katika sekta mbalimbali kama vile ufundi, kilimo, uvuvi, muziki na michezo.
Aidha, ametoa wito kwa wazazi na wawekezaji kuunga mkono elimu hiyo kwa kuwa ni suluhisho muhimu kwa changamoto ya ukosefu wa ajira na inahitajika kwa ufanisi wa sekta ya uwekezaji.
Prof. Mkenda ameyasema hayo , katika Mkutano wa Umoja wa Maafisa Elimu wa Mikoa na Halmashauri uliofanyika jijini Dar es Salaam.
Ameeleza kuwa shule za amali zitakazokuwa na rasilimali na vitendea kazi vya kutosha zitapata kibali cha kufundisha na kutoa mafunzo ya vitendo.
Pia, amesisitiza kuwa elimu ya amali inapaswa kuimarishwa ili kukabiliana na upungufu wa wafanyakazi wenye ujuzi katika sekta mbalimbali za uchumi.
"Wazazi kumsihofie kupeleka watoto wenu katika shule za amali, elimu hii ni fursa muhimu ya kuwajengea watoto maisha bora na mustakabali mzuri wa ajira,"amesema.

Halmashauri zatakiwa kupima maeneo ya huduma za afya na kupata hati miliki
Mkurugenzi wa Idara ya Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI, Dkt. Rashid Mfaume, amezitaka Mamlaka za Serikali za Mitaa kuhakikisha zinapima ardhi za Zahanati, Vituo vya Afya, na Hospitali zote nchini ili kupata hati miliki za maeneo hayo.
Dkt. Mfaume ametoa ushauri huo alipokuwa katika ziara ya ukaguzi wa huduma za afya, lishe, na ustawi wa jamii katika Mkoa wa Dodoma, ambapo alitembelea Kituo cha Afya Kibakwe kilichopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa.
“Ni lazima tupime maeneo yetu, tuweke mipaka rasmi na kuhakikisha yanakuwa na hati miliki ili kuzuia uvamizi na kuimarisha utoaji wa huduma za afya,” amesema Dkt. Mfaume.
Ameongeza kuwa kasi ya ukuaji wa miji inasababisha watu kuhamia karibu na vituo vya huduma, hivyo upimaji wa maeneo hayo utasaidia kulinda miundombinu ya afya dhidi ya uingiliaji usio rasmi.

Dkt. Mfaume: TAMISEMI tumejipanga vyema utekelezaji wa sheria ya Bima ya Afya kwa Wote
Mkurugenzi wa Idara ya Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI, Dkt. Rashid Mfaume, amesema kuwa katika kuelekea utekelezaji wa Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote, TAMISEMI imejipanga vyema kuhakikisha kunakuwa na usimamizi bora huduma za afya katika ngazi ya msingi.
Dkt. Mfaume ametoa kauli hiyo alipokuwa katika ziara yake ya kukagua utoaji wa huduma za afya, lishe, na ustawi wa jamii mkoani Dodoma, ambapo alitembelea Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa.
Amesema TAMISEMI itahakikisha katika ngazi ya afya ya msingi bidhaa zote muhimu za afya zinapatikana.
"Tunawahakikishia Watanzania kuwa katika ngazi ya huduma za afya ya msingi, Ofisi ya Rais TAMISEMI imejipanga kuhakikisha wananchi wote wanaojiunga na Bima ya Afya kwa Wote wanapata huduma zote stahiki kama inavyotakiwa," amesema Dkt. Mfaume.
Aidha, amebainisha kuwa hapo awali kulikuwapo na changamoto ya baadhi ya wanachama wa bima ya afya kukosa dawa katika vituo vya kutolea huduma na kulazimika kununua dawa hizo wenyewe.
Hata hivyo, kwa sasa TAMISEMI imechukua hatua kuhakikisha vituo vya afya vinakuwa na akiba ya kutosha ya dawa na vifaa tiba ili kuboresha huduma kwa wananchi

Wagonjwa 6,847 watibiwa hospitali ya wilaya Handeni
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Mohamed Mchengerwa amesema wagonjwa wapatao 6,846 wamepata huduma za Afya Katika Hospitali ya Wilaya ya Handeni tangu ilipokamilika na kuanza kutoa huduma.
Waziri Mchengerwa ameyasema hayo wakati wa uzinduzi wa Hospitali hiyo iliyozinduliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa katika siku ya kwanza ya ziara yake mkoani Tanga.
Amesema ujenzi wa hospitali hiyo umegharimu jumla ya shilingi Bilioni 7.3 ambapo Serikali imetoa kiasi cha shilingi Bilioni 4.3 na wadau wa Islamic Help wametoa kiasi cha shilingi Bilioni 3.
Amesem mpaka sasa jumla ya majengo yaliyokamilika ni 15 amesema Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Mkoani Tanga hadi sasa imeshapokea wajawazito 900 na kati yao 300 walijifungua kwa njia ya upasuaji ndani ya miaka mitatu(3).
Rais Samia amefanya uzinduzi wa hospitali hiyo akiwa katika ziara mkoani Tanga ambayo ameanza leo Februari 23, 2025 hadi Machi 1, 2025 kwa lengo la kukagua na kuzindua miradi mbaliambali iliyotolewa fedha na Serikali.

Katimba: Serikali imeendelea kuchukua hatua kupunguza uhaba wa walimu
Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Mhe. Zainab Katimba, amesema serikali inaendelea kuchukua hatua za kukabiliana na upungufu wa walimu kwa kuajiri kila mwaka kulingana na upatikanaji wa fedha, huku kwa sasa ikiwa katika majaribio ya matumizi ya teknolojia ya madarasa janja.
Mhe. Katimba ameyasema hayo leo, Februari 22, 2025, alipokuwa akizungumza na Maofisa Elimu Kata waliokuwa wakipatiwa mafunzo ya matumizi ya Madarasa Janja katika Taasisi ya Elimu Kibaha, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kutembelea taasisi zilizo chini ya Ofisi ya Rais – TAMISEMI.
Amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inaendelea kuajiri walimu kila mwaka kwa kutoa vibali vya ajira, huku ikiimarisha utaratibu wa kuwatumia walimu wa kujitolea.
"Watanzania wamehamasika kupeleka watoto shule, na udahili wa wanafunzi umeongezeka maradufu, hali iliyosababisha upungufu wa walimu. Hivyo, serikali, pamoja na kuajiri, imebuni teknolojia ya kutumia madarasa janja, na kwa sasa ipo katika hatua za majaribio," amesema.
Pia, Mhe. Katimba amebainisha kuwa pamoja na jitihada hizo, serikali inaendelea kupandisha madaraja ya walimu kama sehemu ya motisha ya kiutendaji.

Wadau wahimizwa kuzingatia usawa wa kijinsia kwenye miradi ya maendeleo
Mkurugenzi Msaidizi wa Huduma za Ustawi wa Jamii katika Idara ya Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii kutoka Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Subisya Kabuje, ametoa wito kwa wadau wanaotoa misaada kwa wanawake na vijana wa kike kuhakikisha wanawahusisha pia vijana wa kiume na wanaume katika vikundi vya maendeleo ili kuimarisha ustawi wa familia na kuchochea maendeleo ya kiuchumi.
Kabuje ametoa kauli hiyo alipofanya ziara ya kukagua shughuli mbalimbali zinazotekelezwa na Shirika la Brac Maendeleo katika Wilaya ya Singida Vijijini, mkoani humo.
Ameeleza kuwa vikundi hivyo vimekuwa vikipatiwa elimu na misaada mbalimbali, ikiwemo mafunzo ya ujasiriamali, ufugaji na usimamizi wa fedha, ili kusaidia familia zenye kipato cha chini kujikwamua kiuchumi.
Aidha, amesisitiza umuhimu wa wataalamu wa maendeleo ngazi ya mkoa, halmashauri na vijiji kushiriki kikamilifu katika kusimamia uwekezaji wa miradi hiyo, kwani inasaidia jamii kupambana na umaskini.
Vilevile, Kabuje amewahimiza wazazi kuanzisha vituo vya kijamii vya kulelea watoto wadogo walio chini ya miaka mitano ili kuwasaidia wakati wanapokuwa kwenye shughuli za biashara au kilimo. Vituo hivyo vitatoa huduma muhimu za lishe, afya, ulinzi na ujifunzaji wa awali kwa watoto.
Kwa upande wake, Meneja wa Mradi huo, Rachel Mbwiliza, amesema mradi huo unalenga kusaidia watu wa rika mbalimbali, huku hatua ya awali ikitekelezwa katika Halmashauri za Wilaya ya Manyoni, Chamwino, na Singida Vijijin

Katimba:Serikali itawafikia vijana wapate elimu ya kudhibiti maambukizi ya VVU
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais – TAMISEMI Mhe. Zainab Katimba amesema Ofisi hiyo itaendelea kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu na wadau wa maendeleo kuhakikisha inawafikia vijana na kutoa Elimu ya tahadhari na Udhibiti wa maambukuzi ya Virusi vya UKIMWI katika jamii.
Mhe. Katimba ametoa kauli hiyo kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI Mhe. Mohamed Mchengerwa katika hafla ya uzinduzi wa awamu ya tatu ya mradi wa Timiza Malengo ambao ni sehemu ya utekelezaji wa kampeni ya Tunasonga na Samia kutokomeza UKIMWI, katika uwanja wa Madini wilaya ya Ruangwa Mkoa wa Lindi.
Amesema mradi huo unalenga kumuelimisha kijana katika kujitambua na kuweza kujilinda na changamoto zinazochochea katika kujihusisha na tabia hatarishi zinazopelekea kupata maambukizi hasa ya virusi vya UKIMWI.
Aidha, Mhe. Katimba amewapongeza watendaji wote kwenye mradi huo hasa watumishi wa OR – TAMISEMI walioko kwenye Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa kutoka Mikoa 10 na halamshauri 32 kusimamia mradi huo ili uendelea kuleta tija kwa maendeleo ya vijana wa Tanzania.
Kwa upande wake, mgeni Rasmi Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera,Bunge na Uratibu Mhe. Ummy Nderiananga kwa niaba ya Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa, amesema kiwango cha ushamiri wa maambukizi ya UKIMWI kwa umri wa miaka 15-49 kimepungua kutoka asilimia 4.7 kwa mwaka 2017 hadi asilimia 4.4 kwa mwaka 2023.
Akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Afya, Naibu Waziri wa Wizara hiyo Mhe. Godwin Mollel amesema gharama za matibabu kwa waathirika wa UKIMWI ni kubwa hivyo wananchi wanatakiwa kuchukua tahadhari ili kuepuka maambukizi

TAMISEMI yakusudia kuboresha zaidi huduma za macho Sekta ya Afya ya Msingi
Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa – TAMISEMI, imesema itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali katika kuimarisha upatikanaji wa huduma za macho katika sekta ya afya ya msingi, kwa kuhakikisha miongozo na sera zinazoongoza utoaji wa huduma hizo zinaendelea kuboreshwa kwa manufaa ya wananchi.
Hayo yameelezwa leo Februari 20, 2025 jijini Dodoma na katibu Mkuu OR – TAMISEMI Adolf Ndunguru kupitia hotuba yake iliyosomwa na Mkurugenzi wa Idara ya Afya,Ustawi wa jamii,na Lishe Dkt. Rashidi Mfaume katika hafla ya uzinduzi wa mpango wa macho imara, utakaotekelezwa katika mikoa minne ya Arusha, Singida, Tabora na Manyara.
Dkt. Mfaume amesema kutokana na eneo la afya ya macho kupewa kipaumbele cha chini, OR – TAMISEMI kwa kushirikiana na wizara ya Afya, na wadau mbalimbali imejipanga kuhakikisha huduma za macho zinajumuishwa katika mfumo wa afya ya msingi ili kuwafikia watoto wengi zaidi katika jamii.
Naye, Mkurugenzi wa huduma za uuguzi na ukunga Dkt. Ziada Sellah akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama, amesema inakadiriwa kuwa wastani wa watoto nane kati ya kila watoto 10,000 wenye umri wa miaka 0 -15, wana ulemavu wa kutokuona na idadi kubwa zaidi wana upungufu wa kuona.
“Serikali itaendelea kuboresha huduma za Uzazi, Mama na Mtoto ikiwemo za uchunguzi wa macho na kutoa afua sahihi kwa watoto tangu wakiwa tumboni mwa mama zao hadi wanapofika umri wa miaka mitano, kipindi hiki ni muhimu sana kwani ndio matatizo mengi yasababishayo ulemavu wa kutokuona hutokea,” amesema Dkt. Sellah
Awali, akitoa taarifa ya mpango huo, Daktari Bingwa wa macho kutoka Chuo cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili, Prof. Milka Mafwiri amesema lengo la mpango huo ni kupunguza ulemavu wa kutokuona unaozuilika kwa Watoto hapa nchini kwa kujumuisha afua za afya ya macho kwa watoto katika afya ya msingi hususani kwenye huduma za afya ya uzazi, mama na mtoto.
Kwa mujibu wa Prof. Mafwiri mpango huo unaogharimu Sh.Bilioni 4.9 na utatekelezwa kwa muda wa miaka mitano katika halmashauri 16 za mikoa ya Arusha, Singida, Tabor ana Manyara.
Mpango huo uliopewa kaulimbiu ya uoni bora, Maisha bora, unakuja wakati ambao watoto milioni 1.4 duniani, wanakabiliwa na tatizo la kutoona huku nusu ya idadi hiyo wakiwa ni Watoto wanaoishi katika nchi zinazoendelea ikiwamo Tanzania.

Trilioni 1.3/- zatumika kuboresha afya ya msingi nchini
KATIKA kipindi cha miaka minne ya uongozi wa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, kiasi cha Sh.Trilioni 1.3 kimetumika kufanya maboresho makubwa kwenye miundombinu ya kutolea huduma za afya, vifaa na vifaa tiba, dawa na ubora wa utoaji wa huduma za afya ya msingi nchini.
Mkurugenzi wa Idara ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Dkt. Rashid Mfaume ameyasema hayo leo Februari 19, 2025 alipokuwa akizungumzia mafanikio ya miaka minne ya Serikali ya Awamu ya Sita katika utoaji wa huduma za afya ngazi ya msingi nchini.
Amesema fedha hizo zimetumika kufanya uwekezaji katika afya msingi na kuchangia ongezeko la miundombinu ambapo hadi sasa kuna zahanati 6163, vituo vya afya 932 na hospitali za Wilaya 188.
“Mpaka sasa kuna hospitali mpya za Wilaya 129 ambazo zimejengwa kwenye maeneo ya pembezoni, hospitali kongwe 48 zimeboreshwa, vituo vya kutolea huduma za afya 367 vyenye uwezo wa kufanya upasuaji, kuongeza, damu,” amesema.
Dkt. Mfaume amesema uwekezaji huo umesaidia kupunguza vifo vya mama na mtoto kutoka vizazi hai 556 hadi 104 katika kila vizazi hai 1000.
Pia, amesema katika maeneo ya vijijini kulikuwa na changamoto kubwa ya kupeleka watumishi wa afya na ilitokana na kutokuwa na nyumba za kuishi lakini mpaka sasa Serikali imejenga nyumba 270 kwa ajili yao.
Pamoja na hayo, amesema Serikali imejenga majengo ya kutolea huduma za dharura 86, magari ya kubebea wagonjwa 382 yamesambazwa kwenye halmashauri zote huku kwa kipindi hicho watumishi 25,936 wameajiriwa.

Katimba atoa maelekezo kwa chuo cha hombolo kuwajengea uwezo viongozi wa mitaa na vijiji
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais-TAMISEMI Mhe. Zainab Katimba ametoa maelekezo kwa Chuo cha Serikali za Mitaa Hombolo kuwasiliana na Wakurugenzi Halmashauri zote nchini ambazo hazijatimiza maelekezo ya serikali ya kutoa mafunzo ya kuwajengea uwezo viongozi wa serikali za mitaa na vijiji ili wawezeshe kupata mafunzo hayo.
Mhe. Katimba ametoa maelekezo hayo baada ya kutembelea chuo hicho kilichopo Hombolo jijini Dodoma ikiwa ni ziara ya kikazi ya kutembelea taasisi zilizo chini ya Ofisi ya Rais - TAMISEMI kwa lengo la kujitambulisha na kuzungumza na viongozi na watumishi wa taasisi hizo ili kupata mwelekeo wa kiutendaji wa Taasisi hizo.
"Mafunzo haya ni ya lazima sio ya hiari mfanye mawasiliano ili waweze kuhakikisha mafunzo haya yanaweza kufanyika kwa wenyeviti wetu hawa na mafunzo haya mnayotoa yana lengo zuri la kuwajengea uwezo wale watendaji wote waliopo huko kwenye mamlaka za serikali za mitaa waweze kutimiza majukumu yao kwa ufanisi," amesema
Amesisitiza katika mafunzo ya kuwajengea uwezo viongozi yanatakiwa kuendana na mabadiliko ya kifikra ili mamlaka za serikali za mitaa zielewe kuwa pamoja na utoaji wa huduma kwa jamii bali ni chombo cha kuwezesha shughuli za kiuchumi.
"Mamlaka zetu za serikali za mitaa ziwe ni chombo cha kuchochea na kuwezesha wananchi katika shughuli mbalimbali za uzalishaji mali katika sekta mbalimbali najua mna'component' nyingi lakini katika eneo hili natoa msisitizo,"amesema Mhe. Katimba.

Samia bond yaorodheshwa dse
Samia Infastructure Bond hati fungani Mahususi inayotolewa na Benki ya CRDB, kwa ajili ya kufadhili miradi muhimu ya miundombinu nchini Tanzania, hasa ujenzi wa barabara chini ya Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini (TARURA), leo imeorodheshwa kwenye soko la hisa la Dar es Salaam, hatua hiyo imejiri baada ya kukusanywa kiasi cha bilioni 323 kutoka Taasisi mbalimbali na wawekezaji binafsi.
Zoezi hilo limeongozwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhe. Mohamed Mchengerwa kwa kupiga kengele ikiwa ni ishara ya kuorodhesha Samia Infastructure Bond kwenye soko la hisa la Dar es Salaam.
Samia Infastructure Bond inatazamiwa kutatua changamoto ya upatikanaji wa fedha kwa ajili ya malipo ya wakandarasi wanaotekeleza miradi ya barabara hivyo kuharakisha maendeleo ya miundombinu muhimu kwa usafirishaji wa abiria, mizigo na huduma na bidhaa

Waziri mchengerwa akutana na kampuni iliyoonesha nia kulifanya jiji la dar kuwa la kisasa
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI Mhe. Mohamed Mchengerwa amekutana na wawakilishi wa Kampuni ya Straling Holding ya Abu Dhabi na kujadili namna bora ya ujenzi wa mji mpya wa kisasa katika Jiji la Dar es Salaam.
Waziri Mchengerwa amekutana na Kampuni ya Straling Holding leo tarehe 14.02.2025 kwenye ukumbi TAMISEMI jijini Dodoma ambao wameonesha nia ya kuwekeza kwenye ujenzi wa miundombinu ya barabara, madaraja, elimu, afya, bandari, umeme wa maji, reli, mifumo ya umwagiliaji, madini na viwanda nchini.
Mhe. Mchengerwa amefanya kikao kazi na wawekezaji hao ili kuwa na uelewa wa pamoja juu ya shughuli wanazozifanya, ili kuona kama kuna haja ya kushirikiana nao katika ujenzi wa mji mpya wa kisasa katika jiji la Dar es Salaam kwa kuzingatia maslahi mapana ya taifa

Mchengerwa awaweka kikaangoni wakurugenzi watoto kusomea chini ya mti
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa, ameagiza tathmini ifanyike kubaini maeneo ambapo wanafunzi wanalazimika kusoma chini au kukaa chini ya miti.
Pia, amewataka wakurugenzi wa halmashauri na wataalamu wao kuandikiwa barua za kujieleza juu ya hali hiyo.
Agizo hilo limetolewa leo, Februari 13, 2025, jijini Dodoma, wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya kukabiliana na msongo wa mawazo kazini kwa watumishi wa TAMISEMI.
Mchengerwa amesisitiza kuwa haiwezekani katika karne hii wanafunzi wakakosa madarasa au madawati, ilhali serikali imetumia matrilioni ya shilingi kuboresha sekta ya elimu.
"Miaka yote tumekuwa tukipata usumbufu ikifika Desemba na Januari, lazima zitafutwe sh. bilioni 250 au 300 kwa madarasa na madawati. Lakini sasa miaka miwili imepita hatujamuomba Rais fedha za kujenga madarasa au kununua madawati. Msisubiri msukumwe, fanyeni kazi," amesisitiza Mhe. Mchengerwa.
Ameagiza Idara ya Usimamizi wa Elimu ya TAMISEMI kufanya tathmini ya shule zote za msingi na sekondari zilizo chakavu ili kuweka mpango wa ukarabati.
Aidha, amewapongeza watumishi wa TAMISEMI kwa kusimamia uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa ufanisi na kuwataka kuendelea kutoa huduma bora zinazokidhi matarajio ya wananchi.
Kuhusu sekta ya afya, Mchengerwa ameeleza kuwa juhudi za TAMISEMI zimechangia kupunguza vifo vya mama na mtoto, huku akihimiza ufuatiliaji wa karibu kwa waganga wakuu wa mikoa na wilaya ili kuboresha huduma za afya kwa wananchi.
Aidha, amewahimiza watumishi hao kufuatiliwa kwa karibu Waganga Wakuu wa Mikoa na Wilaya na kwenye vituo vya afya ili waongeze kasi ya kuwahudumia wananchi kwa weledi

Tamisemi yaweka wazi viwango vipya ujenzi wa madarasa na zahanati
Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) imefanya mapitio ya bajeti kwa kuzingatia muundo wa kanda na gharama za maisha ili kuhakikisha fedha zinazotengwa kwa miradi ya ujenzi zinatosheleza kukamilisha miundombinu muhimu.
Hivyo, kuanzia bajeti ya mwaka 2024/25, madarasa yatagharimu kati ya Sh.Milioni 22 hadi 25, huku ujenzi wa zahanati ukigharimu kati ya Sh.Milioni 284 hadi 358.
Naibu Waziri wa TAMISEMI, Mhe. Zainab Katimba, ameliambia Bunge leo Februari 13, 2025 alipokuwa akichangia taarifa ya mwaka ya utekelezaji wa majukumu ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC).
Amesema hatua hiyo imetokana na serikali kubaini tofauti kubwa ya gharama za vifaa vya ujenzi kati ya kanda mbalimbali, hali iliyokuwa ikikwamisha utekelezaji wa miradi muhimu kama shule, zahanati na majengo ya utawala.
“Tumefanya maboresho ya bajeti ili kuhakikisha miradi inakamilika kwa viwango sahihi. Kuanzia bajeti ya mwaka 2024/2025, madarasa yatagharimu kati ya shilingi milioni 22 hadi 25, huku ujenzi wa zahanati ukigharimu kati ya shilingi milioni 284 hadi 358,” amesema Mhe. Katimba.
Awali, Mwenyekiti wa Kamati ya LAAC, Mhe. Halima Mdee, amesisitiza kuwa kuanzia mwaka wa fedha 2025/2026, taasisi zote za umma zinazotoa huduma katika Serikali za Mitaa zinapaswa kushirikiana katika kuandaa miundombinu muhimu kama barabara, umeme, na maji kabla ya kuanza miradi yoyote ya ujenzi.

Mchengerwa: Mhe.Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa kipaumbele kwa Serikali za Mitaa kuchochea maendeleo
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa amesema Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameendelea kuweka mkazo katika kuimarisha serikali za mitaa kama chachu ya maendeleo ya wananchi kwa kuongeza rasilimali, kuboresha mifumo ya utendaji, na kuimarisha uwajibikaji wa viongozi wa halmashauri.
Waziri Mchengerwa amesema hayo Machi 11, 2025 kwenye ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa 39 wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT) uliofanyika jijini Dodoma.
“Maendeleo siyo ahadi, bali ni hatua zinazochukuliwa kila siku kwa vitendo. Tunamshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwa mstari wa mbele kuhakikisha serikali za mitaa zinakuwa msingi wa maendeleo ya wananchi. Serikali yake imeonesha kuwa maendeleo yanaanzia chini kwenda juu, na kwa kuimarisha serikali za mitaa, tumewawezesha wananchi kushiriki moja kwa moja katika mchakato wa maendeleo,” amesema Mhe. Mchengerwa.
Ameeleza kuwa uwekezaji mkubwa umefanyika katika sekta ya elimu, afya, na miundombinu, hatua inayowezesha wananchi kushiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi.
Aidha, Waziri Mchengerwa amewahimiza viongozi wa serikali za mitaa kuwa wabunifu, kuzingatia uadilifu katika utendaji wao, na kushirikiana na serikali kuu ili kuhakikisha maendeleo ya taifa yanapiga hatua kwa kasi zaidi.

TAMISEMI yakemea Wanasheria wa Halmashauri wasiowajibika
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Mhe. Zainab Katimba, amewataka wakuu wa Idara na Vitengo vya Sheria katika Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kuhakikisha wanazingatia weledi, uadilifu, na uwajibikaji katika majukumu yao ili kuepusha uzembe unaoigharimu serikali.
Akizungumza Februari 12, 2025 kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa, wakati wa ufunguzi wa kikao kazi cha siku mbili cha wakuu wa idara hizo jijini Dodoma, Mhe. Katimba amesema kuna uzembe wa hali ya juu katika usimamizi wa mashauri ya madai.
"Katika baadhi ya maeneo, mashauri ya madai yameendeshwa upande mmoja kwa zaidi ya miaka mitano na maamuzi kufikiwa dhidi ya serikali bila mwanasheria wa halmashauri husika kuhudhuria hata mara moja mahakamani," amesema.
Ameongeza kuwa serikali haiwezi kuvumilia uzembe huu, hasa pale ambapo halmashauri hulazimika kulipa mabilioni ya shilingi baada ya kushindwa kesi kwa sababu ya kutohudhuria mahakamani au kusimamia vibaya mashauri.
Mhe. Katimba pia amebainisha changamoto katika usimamizi wa mikataba, ambapo baadhi ya mikataba hufikia ukomo bila mamlaka husika kuchukua hatua mapema za kuongeza muda wake, hali inayosababisha utekelezaji wa majukumu nje ya utaratibu wa kisheria.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Huduma za Kisheria Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Wakili Richard Odongo, amesema kikao kazi hicho kinalenga kujadili changamoto hizi na kuweka mikakati madhubuti ya kuongeza uwajibikaji na uadilifu katika sekta ya sheria ndani ya halmashauri.

Meneja tarura kilimanjaro aagizwa ukarabati barabara ya sonu-sawe
Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais – TAMISEMI Mhe. Dkt. Festo Dugange, amemuelekeza Meneja wa Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini (TARURA) Mkoa wa Kilimanjaro kuwasilisha maombi maalumu ya fedha kwa ajili ya ukarabati wa barabara ya Sonu kwenda Sawe ambayo imeharibika kutokana na mvua.
Dkt. Dugange ametoa maelekezo hayo Februari 10, 2025 alipokuwa akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Hai, Mhe. Saashisha Mafuwe aliyetaka kujua ni lini serikali itakarabati barabara hiyo ili iweze kupitika wakati wote.
Akijibu swali hilo kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa, Dkt. Dugange alisema: "Namuelekeza Meneja wa TARURA mkoa wa Kilimanjaro na Meneja wa TARURA Wilaya ya Hai, kama hawajawasilisha maombi maalumu na tathmini ya mahitaji ya fedha, wafanye hivyo mara moja ili serikali ipeleke fedha kwa ajili ya kuirekebisha barabara hiyo."
Katika swali la msingi, Mbunge wa Kishapu, Mhe. Boniphace Butondo, amehoji lini serikali itapeleka fedha za dharura wilayani Kishapu kwa ajili ya matengenezo ya barabara zilizoathiriwa na mvua za El Nino mwaka 2023/24.
Dkt. Dugange akijibu swali hilo, amefafanua kuwa serikali tayari imepeleka sh. milioni 190 katika mwaka wa fedha 2023/24 kwa ajili ya matengenezo ya dharura kwenye baadhi ya maeneo, ikiwemo barabara ya Mwamakanga – Mwanghiri yenye urefu wa kilomita 4.5 pamoja na ujenzi wa makalavati saba.
Aidha, ameeleza kuwa TARURA Wilaya ya Kishapu inasimamia mtandao wa barabara wenye urefu wa kilomita 1,024.66, ambapo kilomita 2 ni za lami, kilomita 405.64 ni za changarawe, na kilomita 617.02 ni za udongo. Katika tathmini ya mwaka 2023/24, serikali ilibaini kuwa Sh.Bilioni 2.55 zinahitajika kwa ajili ya ukarabati wa barabara hizo.
Dkt. Dugange amesisitiza kuwa serikali itaendelea kutekeleza matengenezo ya barabara zote zilizoathiriwa na mvua, kulingana na upatikanaji wa fedha.

Mkandarasi anayejenga barabara za tactic morogoro atakiwa kukamilisha kazi ndani ya miezi mitatu
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) anayeshughulikia Miundombinu, Mhandisi Rogatus Mativila amemtaka Mkandarasi M/s Jiangxi GEO Engineering Group anayejenga barabara ya Kihonda - VETA yenye urefu wa Km 12.85 kwa kiwango cha lami Manispaa ya Morogoro mkoani Morogoro kufanya kazi usiku na mchana ili kukamilisha ujenzi wa barabara hiyo kwa ubora unaotakiwa ndani ya miezi mitatu hadi kufikia mwezi Mei 2025.
Mhandisi Mativila ametoa agizo hilo kwa mkandarasi pamoja na Mhandisi Mshauri wa mradi huo katika ziara ya ukaguzi wa mradi huo unaotekelezwa kupitia Mradi wa Uboreshaji wa Miji Tanzania (TACTIC) chini ya mkopo nafuu toka Benki ya Dunia.
“Nimekuja kutembelea moja ya miradi mikubwa ambayo serikali ya awamu ya sita inatekeleza kwa ajili ya kuleta maendeleo na ushindani katika miji 45 ya Tanzania iliyochanguliwa iwe na ushindani wa kuwa na miundombinu bora ikiwemo ya barabara kwa kiwango cha lami inayowezesha kukua kwa uchumi’’, alisema.
Alisema kati ya miji hiyo ni pamoja na Manispaa ya Morogoro ambayo inanufaika na utekelezaji wa mradi huo mkubwa ambapo kwa mkoa huo mradi unagharimu kiasi cha shilingi bilioni 19.6.
“Mradi huu umechelewa na upo nyuma kwa asilimia 18 na kwamba umetekelezwa kwa asilimia 82 tu na kuna sababu kadhaa ambazo zimeelezwa, baada ya kuweka mambo sawa tunataka mradi huu ukamilike ndani ya muda wa miezi mitatu endapo kukiwa na mvua kubwa basi mradi uwe umekamilika Mwezi Augosti mwaka huu“, alisema .
Naye, Meneja wa TARURA Wilaya ya Morogoro, Mhandisi Mohamed Muanda alisema ujenzi wa mradi huo ulianza Oktoba 23, 2024 na kutakiwa kukamilika Februari 2025 ambapo awamu ya kwanza inahusisha ujenzi wa mifereji mikubwa ya maji ya mvua kuelekea mto Kikundi yenye urefu wa jumla ya Km 4.4, ujenzi wa ofisi ya Mhandisi Mshauri na ofisi ya wasimamizi wa miradi.
Kwa upande wake, Mwakilishi wa Mhandisi Mshauri kutoka nchini pamoja na Mhandisi Mshauri kutoka Ethiopia (JV Core consultancy), Mhandisi Dargie Dilbedi alimhakikishia Naibu Katibu kwamba kazi hiyo ipo katika hatua ya mwisho na kwamba anatumaini ndani ya miezi mitatu ya nyongeza itakamilika.

Kamati ya bunge yaelekeza halmashauri zenye mapato makubwa kujenga uzio maeneo ya huduma za afya
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya TAMISEMI, imeielekeza Ofisi ya Rais – TAMISEMI kuhakikisha Halmashauri zote nchini zenye mapato makubwa ya ndani zinajenga uzio katika maeneo ya kutolea huduma za afya kwa ajili ya usalama wa wananchi na mali za umma.
Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Justin Nyamoga ametoa maelekezo hayo wakati wa ukaguzi wa miradi ya maendeleo ya elimu na afya katika Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha, Mkoa wa Pwani.
“Tukipita kwenye maeneo mengi tunaona hospitali hazina uzio. Kutokana na maeneo mengi kuwa karibu na makazi ya watu, Kamati inashauri Halmashauri zenye mapato ya ndani ya kutosha zianze kujenga uzio kwenye maeneo ya huduma za jamii kama haya,” amesema Mhe. Nyamoga.
Ameongeza kuwa ni muhimu maeneo yanayotoa huduma za afya kuwa salama na kuhakikisha faragha kwa wagonjwa na wateja wanaoingia na kutoka.
Pamoja na hilo, Mhe. Nyamoga amezitaka Halmashauri zote nchini kufuata miongozo na taratibu katika matumizi ya fedha za miradi ya BOOST na SEQUIP, ili Watanzania waendelee kunufaika na juhudi za Serikali katika kuimarisha sekta ya elimu.
Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Mhe. Zainab Katimba, amepokea maelekezo hayo huku akisisitiza umuhimu wa Halmashauri kuendeleza miundombinu katika sekta nyeti, ikiwamo sekta ya afya.
Kamati hiyo imemaliza ziara yake ya siku mbili katika Mkoa wa Pwani, ambapo imetembelea na kukagua miradi ya maendeleo katika Halmashauri ya Mji wa Rufiji na Manispaa ya Kibaha.

Kamati ya bunge yapongeza rufiji kwa utekelezaji bora wa miradi
KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya TAMISEMI, imeridhishwa na utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika Wilaya ya Rufiji, hususan ukarabati wa Hospitali ya Wilaya pamoja na miradi mingine ya afya, elimu, miundombinu na masoko.
Mwenyekiti wa kamati hiyo, Mhe. Justin Nyamoga ameyasema hayo atika ziara ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa miradi ya afya, elimu, soko, jengo la utawala na miundominu ya barabara za TARURA inayotekelezwa na Ofisi ya Rais-TAMISEMI.
Mhe. Nyamoga amepongeza usimamizi mzuri wa miradi hiyo, akibainisha kuwa Rufiji imeonyesha mfano bora wa utekelezaji wa miradi ya maendeleo.
"Mhe. Waziri, tumejionea kazi nzuri ya ukarabati wa hospitali ya Wilaya ya Rufiji. Tumefurahishwa na ubora wa mradi huu, hivyo tunakupongeza kwa usimamizi mzuri. Rufiji ni mfano wa kuigwa," amesema Mhe. Nyamoga.
Aidha, Mjumbe wa Kamati hiyo, Mhe. Salome Makamba, ameeleza kuwa licha ya hospitali hiyo kujengwa mwaka 1963, ukarabati wake umefanyika kwa kiwango cha hali ya juu, jambo linaloonyesha utekelezaji mzuri wa miradi ya serikali.
Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais-TAMISEMI (Elimu), Mhe. Zainab Katimba, ameeleza kuwa katika kipindi cha miaka minne ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, serikali imewekeza zaidi ya Sh.Trilioni 1.2 katika sekta ya afya, huku Rufiji pekee ikinufaika na uwekezaji wa Sh.Bilioni 8.3.
Mbunge wa Jimbo la Rufiji, ambaye pia ni Waziri wa TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa, ameeleza kuwa pamoja na maboresho ya huduma za afya, Rufiji inaendelea kuwekeza katika miradi mikubwa ya maendeleo, ikiwamo ujenzi wa kiwanda kikubwa cha sukari, kiwanda cha ndizi kinachotarajiwa kutoa ajira zaidi ya 8,000, pamoja na ujenzi wa bandari ndogo ya Muhoro kwa ajili ya kusafirisha bidhaa za kilimo.
Ziara ya Kamati hiyo wilayani Rufiji ilihitimishwa kwa ukaguzi wa miradi mbalimbali, ikiwamo soko la Umwe, jengo la Halmashauri ya Mji, barabara za TARURA, na Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Mkoa wa Pwani – Bibi Titi Mohamed.

Anwani za makazi zaboresha usafirishaji wa dawa na vifaa vya shule nchini
Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe. Dkt. Festo Dugange, amesema kuwa mfumo wa anwani za makazi umeleta mapinduzi makubwa katika usambazaji wa dawa kwenye vituo vya kutolea huduma za afya ya msingi nchini, kwani hakuna tena changamoto ya kutafuta au kuuliza eneo la zahanati au kituo cha afya kilipo.
Akizungumza leo Februari 8, 2025 kwenye kilele cha maadhimisho ya Wiki ya Anwani za Makazi jijini Dodoma, Dkt. Dugange ameeleza kuwa pamoja na dawa, mfumo huu pia umewezesha vifaa na mahitaji muhimu ya shule kufikishwa katika maeneo husika kwa ufanisi mkubwa zaidi kuliko ilivyokuwa kabla ya utekelezaji wa mfumo huo.
Aidha, amebainisha kuwa Bohari ya Dawa ya Taifa (MSD) sasa inasambaza dawa moja kwa moja hadi kwenye zahanati katika maeneo yote ya Tanzania kwa kutumia anwani za makazi, jambo ambalo limeimarisha usambazaji wa dawa na huduma za afya kwa wananchi wa mijini na vijijini kwa kiwango kikubwa.
Dkt. Dugange amesisitiza kuwa mfumo wa anwani za makazi umewezesha maeneo yote nchini kufikika kwa urahisi zaidi, na Ofisi ya Rais - TAMISEMI itaendelea kusimamia na kuhakikisha utekelezaji wake unazidi kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi.

Mkandarasi anayejenga barabara za tactic jijini dodoma atakiwa kukamilisha ujenzi kwa wakati
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) anayeshughulikia miundombinu, Mhandisi Rogatus Mativila amemuagiza Mkandarasi M/s China Geo-Engineering Corporation kuhakikisha anakamilisha ujenzi wa barabara kiwango cha lami Km 10.21, mtaro wa maji ya mvua Ilazo Km 2.1, uboreshaji wa mabwawa ya kuhifadhi maji ya mvua (3), mitaro ya kutiririsha maji Km 2.81 pamoja na ujenzi wa jengo la usimamizi na uratibu wa miradi kwa wakati na ubora.
Mhandisi Mativila ametoa agizo hilo alipokuwa katika ziara ya ukaguzi wa miradi hiyo jijini Dodoma ambayo inatekelezwa kupitia Mradi wa Uboreshaji wa Miji Tanzania (TACTIC) chini ya mkopo nafuu toka Benki ya Dunia.
Naibu Katibu Mkuu ameeleza kuwa baada ya ukaguzi wa mradi huo amebaini kuwa ujenzi wa barabara, mifereji ya maji ya mvua pamoja na jengo la usimamizi na uratibu wa miradi upo nyuma ya muda kutokana na nguvu kazi hafifu, ukosefu wa vitendea kazi na kupelekea mradi huo ambao unapaswa kukamilika Februari 2025 kuonyesha ishara za kutofikia malengo ya kukamilika kwa muda na kuwanyima wananchi fursa ya kupata huduma ya barabara.
“Mradi upo asilimia 45% tu bado zimebaki 55% kazi kukamilika, mpaka leo zimebaki siku 13 tu ili mkataba ukamilike. Tumeongea na mkandarasi lakini tumeona sehemu kubwa ya ucheleweshaji wa kazi umesababishwa na mkandarasi mwenyewe kwa kushindwa kuweka nguvu kazi na vifaa vya kutosha, ametueleza anahitaji mwaka mwingine ili akamilishe kazi kiukweli ataongezewa muda lakini atapata adhabu ya kukatwa fedha kulingana na mkataba na pia atatakiwa afanye kazi usiku na mchana ili akamilishe kazi ndani ya muda mfupi na kwa ubora ule ule”. amesema

Waziri mchengerwa: muswada wa makao makuu dodoma uingie bungeni haraka
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe. Mohammed Mchengerwa, amemuelekeza Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo kuhakikisha Muswada wa Sheria ya Usimamizi na Uendelezaji wa Makao Makuu Dodoma unawasilishwa bungeni kabla ya kuvunjwa kwa Bunge la 12 mwaka huu.
Mhe. Mchengerwa ametoa agizo hilo leo, Februari 6, 2025 katika hafla ya utiaji saini wa mkataba wa ujenzi wa Soko Kuu la Majengo na vituo vya daladala jijini Dodoma kupitia mradi wa uboreshaji miundombinu ya Miji (TACTIC) awamu ya pili unaotekelezwa chini ya Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (TARURA).
Amesema Dodoma haiwezi kuwa Makao Makuu kwa matamko pekee, bali ni lazima kuwe na sheria rasmi itakayohakikisha hadhi yake inalindwa kwa vizazi vijavyo.
Amesema "Sheria hii iharakishwe kama zinavyoharakishwa sheria nyingine. Hatuwezi kusubiri tena. Tutamuomba Mheshimiwa Rais kwa hati ya dharura ili iwasilishwe bungeni kabla ya kuvunjwa kwa Bunge hili."

Majaribio ya utoaji wa barua za utambulisho kupitia napa yaonesha mafanikio
Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa – TAMISEMI imesema majaribio ya utoaji wa barua za utambulisho kwa njia ya kidijitali kwa kutumia mfumo wa anuani za makazi (NAPA) yameonesha mafanikio katika kurahisisha utoaji na upokeaji wa huduma za utambuzi.
Hayo yameelezwa leo Februari 6, 2025 na Naibu Waziri OR – TAMISEMI Dkt. Festo Dugange wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma katika uzinduzi wa wiki ya anuani za makazi kwa mwaka 2025 inayoenda sambamba na maonesho ya huduma mbalimbali zinazotolewa kupitia huduma ya mtandao kwa kutumia anuani za makazi.
Kwa mujibu wa Dkt. Dugange mbali na mafanikio makubwa yaliyo onekana katika hatua za awali za majaribio, mfumo huo wa NAPA umesaidi katika utekelezaji wa jukumu la kutoa majina ya mitaa na kugeuka nyenzo muhimu zaidi inayorahisisha utambuzi wa makazi, utoaji na upokeaji wa huduma mbalimbali.
Kutokana na ufanisi huo, Dkt. Dugange amewaelekeza Makatibu Tawala wa Mikoa na Wakurugenzi wa Halmashauri kuwaruhusu, kuwahamasisha na kuwahimiza waratibu wa mfumo huo katika maeneo yao kushiriki mafunzo ya mara kwa mara yanayolenga kuboresha utoaji wa huduma kupitia mfumo wa NAPA, ili wawe msaada wa kuwawezesha wananchi kutambua anuani zao.
Kadhalika ameeleza kuwa OR – TAMISEMI itaweka mazingira ya kutoa msaada wa kiufundi pale inapohitajika wakati wote, ikiwa ni hatua ya kudhibiti changamoto zinazo weza kujitokeza.
Kwa upande wake waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Jerry William Silaa amepongeza ushirikiano uliopo baina ya wizara hizo mbili akieleza namna unavyorahisha utekelezaji wa mfumo huo wa anuani za makazi.
Maadhimisho ya wiki ya anuani za makazi kwa mwaka 2025 yamebebwa na kauli mbiu ya “Tambua na tumia anwani za makazi kurahisisha utoaji na upokeaji wa huduma”.

Uandikishaji wa wanafunzi ufanyike bila kujali tofauti zao’ mhe mchengerwa
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Mohamed Mchengerwa amewaagiza Viongozi wa Mikoa na Halmashauri zote nchini kuhakikisha uandikishaji wa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari unafanyika bila kujali tofauti zao za kiafya na kimaumbile.
Mhe. Mchengerwa ametoa maagizo hayo leo Januari 6, 2025 wakati wa hafla ya kukabidhi vyumba 18 vya madarasa vilivyogharimu Shilingi milioni 300 katika Halmashauri ya Wiaya ya Bahi ambapo pia ametoa tuzo kwa waandishi 15 wa habari za Mradi wa Shule Bora.
'Nawaagiza mkasimamie kwa dhati zoezi la uandikishaji wa wanafunzi wote bila kujali tofauti zao za kiafya na kimaumbile wenye umri lengwa kwa ajili ya kuanza darasa la awali, msingi na MEMKWA' amesisitiza.
Mchengerwa amewataka Viongozi hao kutoa takwimu sahihi za uandikishaji na jinsi wanavyoripoti wanafunzi katika ngazi ya elimu ya awali, msingi na sekondari kama ilivyoelekezwa na Ofisi ya Rais-TAMISEMI (Kila siku ya Ijumaa katika wiki).
Naye, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule amempongeza Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uwekezaji mkubwa katika Sekta ya Elimu ambayo yameleta matokeo makubwa ikiwemo kuongeza ufaulu Dodoma kwa shule za msingi na sekondari na kupunguza utoro kutoka wanafunzi 24,000 hadi 6,000 (2024).
Akitoa taarifa kuhusu umalizaji wa ujenzi wa madarasa hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Bahi, Zaina Mlawa alisema ujenzi wa madarasa 10 umefanyika kwa kufuata mbinu za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi ili kuboresha mazingira ya ufundishaji na ujifunzaji ambao unalengo la kuboresha mazingira ya ufundishaji na ujifunzaji.
Naye Mwakilishi wa Balozi kutoka ubalozi wa Uingereza, Sally Hedley alisema elimu ni kipaumbele kwa serikali hiyo hivyo nchi hiyo itaendelea kuwekeza katika sekta hiyo kwa kuweka miradi rafiki ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi kwa wanafunzi.
Mradi wa Shule Bora umejikita katika kuboresha elimu ya awali na msingi kwa katika maeneo manne ya ujifunzaji, ufundishaji, ujumuishi na uimarishaji wa mifumo na ulizinduliwa rasmi na Vicky Ford (Parliamentary Under Secretary State-UK) Aprili 4, 2022 katika shule za Msingi Mkoani iliyopo Kibaha- Pwani. Mikoa unapotekelezwa Mradi ni Dodoma, Singida, Pwani, Tanga, Simiyu, Kigoma, Katavi na Rukwa ambapo uchaguzi wa mikoa hii ulizingatia mambo mbalimbali ikiwemo ufaulu usioridhisha wa wanafunzi katika mitihani ya kuhitimu darasa la saba na ile ya upimaji wa darasa la Nne, utoro na mimba za utotoni.

Simamieni miradi kikamilifu na kwa ubora – mhandisi mativila
Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais – TAMISEMI anayeshughulikia Miundombinu, Mhandisi Rogatus Mativila, amewataka Makatibu Tawala Wasaidizi wa Sekta ya Miundombinu katika Sekretarieti za Mikoa kusimamia miradi kikamilifu kwa mujibu wa mikataba ili kuhakikisha zinakuwa na ubora.
Mhandisi Mativila ametoa maelekezo hayo leo Februari 5, 2025 kwenye kikao kazi kilichofanyika jijini Dodoma, kilicholenga kujadili utekelezaji wa miradi ya ujenzi, ukarabati, na matengenezo ya miundombinu katika Mikoa 26, Wilaya 139, na Halmashauri 184 nchini.
"Ubora wa kazi ni jambo la msingi. Kama ni jengo, lijengwe kwa viwango vinavyostahili. Kuna baadhi ya majengo yanapotembelewa na waheshimiwa wabunge, hubainika kuwa hayana ubora," amesisitiza Mhandisi Mativila.
Aidha, amewataka viongozi hao kuwa na mipango thabiti ya muda mfupi, muda wa kati, na muda mrefu ili kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi, kama ilivyokusudiwa na serikali.
Mhandisi Mativila amewasihi kuboresha utendaji wao kwa lengo la kuleta maendeleo ya kiuchumi na kijamii kwa watanzania wa mijini na vijijini.
Naye, Katibu Tawala Msaidizi wa Miundombinu wa Mkoa wa Morogoro, Mhandisi Ezron Kilamhama, ameahidi kushirikiana na wahandisi wa halmashauri kuhakikisha miradi yote inatekelezwa kwa mujibu wa mikataba na kwa viwango vinavyostahili.
Msanifu Majengo wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Chabu Nghoma, amesema wataandaa mpango kazi wa utekelezaji wa miradi kwa ufanisi na kuuwasilisha kwa Ofisi ya Rais – TAMISEMI ndani ya mwezi wa pili kwa ajili ya tathmini.
Ofisi ya Rais – TAMISEMI ina jukumu la kuratibu matengenezo, ukarabati, na ujenzi wa miundombinu ya barabara, majengo, na miundombinu mingine katika ngazi za mikoa, wilaya, na mamlaka za serikali za mitaa.

Miradi yote ngazi ya msingi itangazwe kupitia nest
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Mohamed Mchengerwa amewataka Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa na wakuu wa vitengo vya manunuzi kuhakikisha miradi yote inayotekelezwa kwenye ngazi ya msingi inatangazwa kupitia mfumo wa Nest.
Mhe. Mchengerwa ameyasema hayo wakati akizungumza na Wabunge,Wakurugenzi wa Halmashauri, Makatibu Tawala Wasaidizi Miundombinu na wakuu wa vitengo vya manunuzi kutoka kwenye Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa wakati wa kikao kazi kuhusu mfumo wa Nest kilichofanyika kwenye ukumbi wa wa Mabeyo jijini Dodoma leo tarehe 04.02.2024.
Amesema baada kupata mafunzo haya leo hii nendeni mkabadilike, fuateni Sheria ya Manunuzi, onyesheni mabadiliko hayo kwenye utekelezaji wa miradi na kuanzia sasa miradi yote itangazwe kupitia mfumo wa Nest na si vinginevyo alisisitiza.
Miradi hiyo ikishatangazwa kupitia Nest hakikisheni mnaisimamia kwa Weledi wa hali ya juu na kwa uaminifu ili itekelezwe kwa viwango vinavyotakiwa na thamani ya fedha iweze kuonekana’ amesema!
Aidha Mhe. Mchengerwa aliwataka PPRA kuhakikisha inawajengewa uwezo watumiaji wa mfumo wa Nest katika ngazi za msingi ili kupunguza changamoto zinazojitokeza wakati wa kuomba zabuni mbalimbali.