
Serikali ya kuendelea kujenga miundombinu ya maji shuleni.
Naibu Waziri ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Dkt. Festo Dugange amesema Serikali ina mikakati ya kuendelea kujenga miundombinu ya maji shuleni katika kila bajeti ya fedha ili kuepuka milipuko ya magonjwa na pamoja na kuhakikisha kuwa Ujenzi wa miundombinu ya vyoo unaojumuisha wa miundombinu ya maji tiririka.
Mhe. Dkt Dugange ameyasema hayo wakati wa akijibu swali Mbunge wa Viiti Maalum Mhe Minza Simon Mjika katika kipindi cha maswali na majibu aliyeuliza “Je, Serikali ina mpango gani kujenga miundombinu ya maji shuleni ili kuepuka milipuko ya magonjwa?” katika Bunge la bajeti linaloendelea Jijini Dodoma.
“shule 5,311 za Sekondari zina vyanzo vya maji vya uhakika ambapo shule zenye maji ya bomba ni 2,960, visima shule 1,217 na wanaovuna maji ya mvua ni shule 1,134. Aidha, shule 20,509 za msingi zina vyanzo vya maji ya uhakika ambapo shule zenye maji ya bomba ni 10,965, visima shule 4,966 na shule zinazovuna maji ya mvua ni 4,578.” Amesisitiza.
Amesema pia, Serikali imetoa maelekezo kwa miradi yote ya ujenzi ya vitio vya afya na ujenzi wa shule mpya utajumuisha miundombinu ya maji inayohusisha kuvuna maji ya mvua, kuunganisha na mifumo ya Mamlaka za Maji na kuchimba visima.
Comments
Please sign in to leave a comment.