
Mchengerwa- marc, madc imsiwe watazamaji wa migogoro
OR-TAMISEMI
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa ametoa maelekezo mahususi kwa wakuu wa mikoa na wa wilaya akiwataka kutokuwa watazamaji wa migogoro na walinzi wa misingi ya haki na amani.
Mchengerwa ameyasema hayo wakati akihitimisha hoja ya mapato na matumizi ya Ofisi ya Rais-TAMISEMI na taasisi zake, Tume ya Utumishi wa Walimu, Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa mwaka 2024/25.
“Ninapenda pia kutumia nafasi hii kutoa maelekezo mahsusi kwa Wakuu wa Mikoa na Wilaya, wajikite kikamilifu katika kulinda amani, mshikamano wa kitaifa na ufanisi wa utendaji wa serikali katika maeneo yao.”
“Hamtakiwi kuwa watazamaji wa migogoro bali wazima moto wa chokochoko, na walinzi wa misingi ya haki, maendeleo na umoja wa kitaifa. Utulivu wa nchi unaanza pale ambapo viongozi wa chini wanatimiza wajibu wao bila kusubiri maagizo kutoka juu.” amesema Mchengerwa
Amewataka kuwasha mwenge wa ulinzi wa jamii na kuzima cheche za migogoro midogo inayoweza kuwa moto mkubwa wa Taifa.
Comments
Please sign in to leave a comment.