
GEITA YAENDELEZA UBABE KIKAPU WASICHANA
Timu ya Mpira wa Kikapu Wasichana kutoka Mkoa wa Geita, imeendelea kufanya vizuri katika Mashindano ya Umoja wa Michezo na Taaluma Tanzania kwa Shule za Msingi yanayofanyika kitaifa mkoani Iringa.
Katika mchezo wa kwanza uliochezwa asubuhi ya leo Tarehe 12 Juni 2025, katika viwanja vya Kichangani, Geita iliichapa Manyara kwa Vikapu 32-7.
Mchezo mwingine ulizikutanisha timu za mikoa ya Dar es Salaam na Mbeya, uliomalizika kwa Mbeya kukubaki kipigo cha jumla ya Vikapu 8-19.
Wenyeji wa UMITASHUMTA kwa mwaka uliopita 2024 Mkoa wa Tabora, nao waliendelea kujiimarisha katika hatua ya makundi, kwa kuiadhibu Songwe na kupata ushindi wa 19-8.
Mchezo wa Mpira wa Kikapu unachezwa kwa mara ya pili katika mashindano ya UMITASHUMTA, ukiwa ulianza rasmi katika mashindano ya mwaka uliopita 2024, huku timu ya Mkoa wa Arusha ikiwa ndio mabingwa watetezi kwa upande wa Wasichana.
Mashindano haya ya UMITASHUMTA na yale ya UMISSETA,yanaratibiwa na Ofisi ya Rais-TAMISEMI,ikishirikiana na Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia pamoja na Wizara ya Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo.
Comments
Please sign in to leave a comment.