
KILIMANJARO, RUVUMA NA NJOMBE MABINGWA RIADHA MAALUMU UMITASHUMTA 2025
Wakimbiaji kutoka mikoa ya Kilimanjaro,Njombe na Ruvuma,wameng'ara katika mchezo wa riadha maalumu (Wasichana na Wavulana) katika mashindano ya Umoja wa Michezo na Taaluma Tanzania kwa Shule za Msingi.
Mchezo wa riadha umeanza rasmi leo juni 11,2025 kwenye viwanja vya Chuo cha Ualimu Kleruu Manispaa ya Iringa, ambapo mashindano ya UMITASHUMTA na UMISSETA yanafanyika Kitaifa mwaka huu.
Katika mbio za leo upande wa Wasichana Mita 100 maalumu, Neema Efrahim kutoka Kilimanjaro na Careen Mohamed kutoka mkoa wa Mwanza, waliongoza wakifuatiwa na Martha Emmanue kutoka Songwe na Pendo Mohamed wa Singida.
Nao wavulana Mita 100 maalumu waliongozwa na Atumani Muhagama kutoka Mkoa wa Ruvuma, akifuatiwa na Edward Kimai wa Mkoa wa Mara huku Yohana Robert wa Dodoma akimaliza katika nafasi ya tatu.
Mratibu wa Mchezo wa riadha katika UMITASHUMTA & UMISSETA 2025 Neema Chongolo, amesema kuwa wanatarajia ushindani mkubwa kama ambavyo imekuwa katika miaka iliyopita.
"Kama unavyojua riadha huwa inakuwa na ushindani mkubwa kutokana na maandalizi ambayo inafanywa na mikoa wanapotoka wanamichezo, kwa hiyo mwaka huu pia tutarajie hivyohivyo" amesema Neema
Kuhusu riadha maalumu amesema mwaka huu mikoa imehamasika kuleta wachezaji wengi, jambo linalodhihirisha kuendelea kukua kwa mchezo wa riadha kwenye UMITASHUMTA.
Comments
Please sign in to leave a comment.