
Mtwara Wasichana Yaendeleza Ubabe UMITASHUMTA 2025
Na OR-TAMISEMI
Timu ya mpira wa wavu ya wasichana kutoka mkoa wa Mtwara ambao ni mabingwa watetezi imeanza kwa kishindo kampeni yake ya kutetea ubingwa katika mashindano ya UMITASHUMTA 2025.
Mtwara imeonesha dhamira ya kutetea ubingwa baada ya kuibuka na ushindi wa seti 3-1 dhidi majirani zao mkoa wa Lindi katika mchezo wa kusisimua uliochezwa kwenye viwanja vya Kleruu, Iringa.
Mtwara walionyesha kiwango cha juu na kujiamini tangu mwanzo, na kushinda seti ya kwanza mabla ya Lindi kujibu mapigo na kusawazisha kwa kuchukua seti ya pili.
Hata hivyo uhodari na umakini wa Mtwara uliamua hatma ya mchezo, wakichukua seti mbili zilizofuata na hivyo kuibuka na ushindi wa jumla wa 3-1.
Katika michezo mingine ya ufunguzi, timu ya wavulana ya Kilimanjaro iliwaduwaza Tabora kwa ushindi wa seti 3-0, ikionyesha kiwango bora na kasi ya hali ya juu,huku wenyeji Iringa ikiungwa mkono na mashabiki wake wa nyumbani, iliibuka kidedea dhidi ya Kagera kwa ushindi wa seti 3-1, katika mchezo mwingine uliovutia mashabiki wengi.
Mashindano ya UMITASHUMTA 2025 yanaendelea kesho kwa michezo mingine ya makundi, ambapo kila timu itakuwa vitani kuwania nafasi ya kufuzu hatua za michuano
Comments
Please sign in to leave a comment.