
SERIKALI ITAENDELEA KUTENGA BAJETI KWA AJILI YA UNUNUZI WA MAGARI YA WAGONJWA.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Zainab Katimba amesema Serikali itaendelea kutenga bajeti kwa ajili ya ununuzi wa magari ya wagonjwa kwa ajili ya vituo vya kutolea huduma za afya nchini.
Mhe. Katimba ameyasema hayo wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum Minza Simon Mjika, katika kipindi cha Maswali na Majibu aliyeuliza “Je, lini Serikali itapeleka Magari ya Wagonjwa katika Vituo vya Afya Ilamba Ndogo na Mwasengela - Meatu.?”
“katika mwaka 2023/24 Halmashauri ya Wilaya ya Meatu imepokea magari 3 ya kubebea wagonjwa na kupelekwa Hospitali ya Wilaya ya Meatu, ambapo magari mawili ya kubebea wagonjwa ya Kituo cha Afya Iramba ndogo na Kituo cha Afya Mwansengela yameachwa katika hospitali ya Wilaya ya Meatu kwa muda”
Amesema Magari hayo yatapelekwa kwenye vituo hivyo pindi majengo ya kutolea huduma za upasuaji wa dharura yatakapokamilika magari.
Amesema Serikali imeendelea kuboresha huduma za afya za dharura na rufaa kwa kununua magari ya wagonjwa na kuyapeleka katika vituo vya huduma za afya.
Comments
Please sign in to leave a comment.