
Serikali yatoa Tsh. bilioni 30 kuwezesha ujenzi wa vituo vya afya kata za kimkakati
Serikali imetoa shilingi bilioni 30 kwa ajili ya kuwezesha ujenzi wa vituo vya afya katika maeneo mbalimbali ya kimkakati kwenye majimbo 120 yaliyoainishwa na waheshimiwa wabunge kupitia bunge la Jamahuri ya Muungano wa Tanzania.
Kauli hiyo imetolewa leo (June 02, 2025) bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Dkt. Festo Dugange wakati akijibu maswali ya waheshimiwa wabunge katika kipindi cha maswali na majibu kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais - TAMISEMI Mhe. Mohamed Mchengerwa.
Akijibu swali la nyongeza la Mhe. Dorothy Kilave mbunge wa jimbo la Temeke aliyetaka kujua hatua zilizochukuliwa na serikali katika kujenga kituo cha afya kata ya Sandali jimbo la Temeke Mhe. Dkt. Dugange amesema licha ya serikali kujenga vituo vya afya katika maeneo mbalimbali ya jimbo la Temeke lakini itaendelea kutenga fedha ili kuhakikisha kata zote za kimkakati zinakuwa na vituo vya afya.
“Serikali inaendelea kuboresha huduma za afya kote nchini na niwahakikishie waheshimiwa wabunge kuwa hii ni dhamira ya dhati ya serikali kuhakikisha inasogeza huduma za afya karibu na wananchi na itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya kujenga vituo vya afya katika kata zote za kimkakati”. alisema Mhe. Dkt. Dugange.
Serikali yatoa Tsh. bilioni 30 kuwezesha ujenzi wa vituo vya afya kata za kimkakati.
Serikali imetoa shilingi bilioni 30 kwa ajili ya kuwezesha ujenzi wa vituo vya afya katika maeneo mbalimbali kwenye majimbo 120 yaliyoainishwa na waheshimiwa wabunge kupitia bunge la Jamahuri ya Muungano wa Tanzania.
Kauli hiyo imetolewa leo (June 02, 2025) bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Dkt. Festo Dugange wakati akijibu maswali ya waheshimiwa wabunge katika kipindi cha maswali na majibu kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais - TAMISEMI Mhe. Mohamed Mchengerwa.
Akijibu swali la nyongeza la Mhe. Dorothy Kilave mbunge wa jimbo la Temeke aliyetaka kujua hatua zilizochukuliwa na serikali katika kujenga kituo cha afya kata ya Sandali jimbo la Temeke Mhe. Dkt. Dugange amesema licha ya serikali kujenga vituo vya afya katika maeneo mbalimbali ya jimbo la Temeke lakini itaendelea kutenga fedha ili kuhakikisha kata zote za kimkakati zinakuwa na vituo vya afya.
“Serikali inaendelea kuboresha huduma za afya kote nchini na niwahakikishie waheshimiwa wabunge kuwa hii ni dhamira ya dhati ya serikali kuhakikisha inasogeza huduma za afya karibu na wananchi na itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya kujenga vituo vya afya katika kata zote za kimkakati”. alisema Mhe. Dkt. Dugange.
Comments
Please sign in to leave a comment.
Tangazo la kuitwa kazini ajira za TMCHIP 2025
Mpango Mkakati wa Usimamizi wa Takwimu wa Ofisi ya Rais TAMISEMI - 2024/25 -2028/29
Kanuni za Uchaguzi wa Mwenyekiti wa Kitongoji 2024
Kanuni za Uchaguzi wa mwaka 2024
Tangazo la Uchaguzi