
UJENZI WA UZIO KWENYE SHULE, SERIKALI YAJA NA MKAKATI MAALUM*
OR- TAMISEMI
Serikali imesema tayari imeweka bajeti na michoro (Master Plan) kwa ajili ya ujenzi wa uzio katika shule zote za Hsekondari za mikoa kama hatua ya kuimarisha ulinzi wa mali za shule na usalama wa wanafunzi.
Akijibu maswali kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais– TAMISEMI Mhe. Mohamed Mchengerwa, Naibu Waziri Mhe. Dkt. Festo Dugange ameliambia bunge leo Mei 09,2025 kuwa pamoja na hatua hiyo wakurugenzi wa halmashauri kupitia mapato ya ndani waendelee kutenga fedha za ujenzi wa uzio kwa ajili ya usalama wa wanafunzi na mali za shule kwenye maeneo yao kadiri ya upatikanaji wa fedha.
Naibu Waziri Dugange ametoa maelekezo hayo wakati akijibu swali la Mheshimiwa Dkt. Angelina Mabula mbunge wa jimbo la Ilemela Mkoani Mwanza aliyeuliza kuwa ni lini Serikali itajenga uzio katika Shule za Msingi ambazo hazina uzio maeneo ya Mijini.
Katika majibu yake Naibu Waziri Dkt. Dugange amesema “Katika mwaka 2022/23 na 2023/24 serikali imetoa shilingi bilioni 5.57 kwa ajili ya ujenzi wa uzio katika shule 185 za watoto wenye mahitaji maalumu, lakini pia Vilevile, Mamlaka za Serikali za Mitaa zimekuwa zikitenga fedha kupitia mapato ya ndani kujenga uzio ili kuimarisha ulinzi katika maeneo yenye changamoto za kiusalama.”
Comments
Please sign in to leave a comment.
Tangazo la kuitwa kazini ajira za TMCHIP 2025
Mpango Mkakati wa Usimamizi wa Takwimu wa Ofisi ya Rais TAMISEMI - 2024/25 -2028/29
Kanuni za Uchaguzi wa Mwenyekiti wa Kitongoji 2024
Kanuni za Uchaguzi wa mwaka 2024
Tangazo la Uchaguzi